Saturday, April 19, 2014

KUELEKEA BIG MATCH:SIMBA VS YANGA.updates zote click hapa

**Mzungu wa Yanga atinga mazoezini na jezi Nyekundu**

KATIKA hali ya kustaajabisha, Kocha Mkuu wa

Yanga, Hans van Der Pluijm, juzi alileta

sintofahamu baada ya kutinga mazoezini na

jezi yenye logo ya doti jekundu, ambayo ni

‘nuksi ’ Jangwani.

Mazoezi hayo yalifanyika kwenye Uwanja wa

Ununio, wakijifua kwa ajili ya mtanange wa

heshima dhidi ya watani wao Simba,

utakaopigwa leo kwenye uwanja wa Taifa Dar .

Mholanzi huyo alikuwa ametinga ‘full ’ jezi

nyeusi ya Klabu ya Feyenoord Rotterdam ya

nchini Uholanzi , inayotumia logo yenye doti

jekundu na nyeupe, ambayo ni kinyume na

miiko ya Yanga .

Ikumbukwe kuwa Yanga waliingia katika

mgogoro mkubwa na wadhamini wa Ligi Kuu

Bara, kampuni ya Vodacom , wakikataa kutumia

logo yenye doti jekundu kwa kile kilichoelezwa

na Baraza la Wazee kupitia katibu wao, Ibrahim

Akilimali, kuwa ni nuksi na kuongeza kuwa

katiba yao imeeleza kukataa rangi nyekundu

Jangwani.

Championi ilikuwa shuhuda katika mazoezi ya

Yanga, ambapo Mholanzi huyo hakuonekana

kujali, pengine hofu ikatawala labda wazee

hawajampa utaratibu na miiko ya klabu hiyo .

Feyenoord, ni moja ya timu zenye jina kubwa

nchini Uholanzi , ambayo mastaa wakubwa

akiwemo straika wa Manchester United , Robin

Van Persie, walipitia.

**CCTV kufungwa uwanjani**

KATIKA kuhakikisha ulinzi na usalama

unapatikana katika mechi ya leo Jumamosi kati

ya Yanga na Simba kwenye Uwanja wa Taifa,

jumla ya askari 400 wameandaliwa kwa ajili ya

kuweka usalama huku kukiwa na magari

mawili ya wagonjwa, yaani wale ambao

watazimia au kupata matatizo uwanjani hapo.

Mchezo huo wa watani wa jadi utapigwa leo

katika Uwanja wa Taifa ukiwa ni moja ya mechi

za kufungia msimu wa 2013/ 2014 ambapo

katika mchezo huo , mshindi wa pili ambaye ni

Yanga atakabidhiwa zawadi ya medali .

Akizungumza na Championi Jumamosi ,

Mtendaji wa Bodi ya Ligi , Silas Mwakibinga,

alisema wameandaa askari 400 na ‘Ambulance ’

mbili kwa ajili ya mchezo wa Simba na Yanga

huku ulinzi na usalama ukiwa wa hali ya juu .

Mwakibinga alisema kuwa wamejiandaa vyema

kabisa na michezo ya kufunga ligi kuu ambayo

yote itachezwa kesho katika viwanja

mbalimbali huku bingwa na mshindi wa pili

wakikabidhiwa zawadi zao kesho.

“Tumeandaa askari 400 kwa ajili ya usalama

katika mechi ya Simba na Yanga na ulinzi kwa

jumla umeimarishwa kila kona huku magari ya

kubebea wagonjwa tumeandaa mawili kwa

lolote litakalojitokeza .

“Kwa upande wa watu wa uwanja, wao

wamefunga ‘security ‘ kamera ( CCTV ) pale kwa

usalama zaidi na hiyo ni ya moja kwa moja si

kwa mchezo pekee wa kesho ( leo) , hivyo kila

kitu kinakwenda safi .

“Lakini kwa bingwa , atakabidhiwa zawadi yake

Chamazi ambazo ni kombe na medali za

dhahabu huku mshindi wa pili taifa yeye

atapewa medali zake pia ,” alisema

Mwakibinga.


**Friends of simba wamteka Okwi**

SAA chache kabla ya mechi ya watani , Yanga

dhidi ya Simba, kama kawaida vituko vinazidi

kuongezeka na mshambuliaji Emmanuel Okwi

anazidi kuwa tatizo .

Okwi alikuwa acheze mechi ya leo , akasusa

kwa kuwa anawadai Yanga dola 40,000 (Sh

milioni 64 ), lakini sasa Friends of Simba

wameingilia na kumteka mawazo zaidi kuwa

hana haja ya kucheza mechi ya leo ,

ataangushiwa mzigo wakipoteza.

Rafiki wa karibu wa Okwi amesema mara

nyingi mchezaji huyo amekuwa akijichimbia

katika hoteli anayoishi na hivi karibuni

alizungumza na memba wa kundi la Friends of

Simba linaloaminika kwa mipango ya kisoka na

kupewa ushauri kwamba hana sababu ya

kucheza mechi hiyo.

“Awali Okwi alikuwa apewe dola 20,000

ambazo ni nusu ya zile anazodai ili acheze ,

lakini baadaye mambo yakabadilika, ninafikiri

ametekwa mawazo na wale Friends of Simba.

“Unajua Friends wamerudi Simba, wanataka

kukiimarisha kikosi chao na ndiyo wametoa

msaada kuipeleka Simba Zanzibar na mmoja

wa mabosi wao ( Zacharia) Hans Pope ndiye

amelipa mshahara wa wachezaji wote maana

waligoma,” kilieleza chanzo kutoka Yanga .

“Kwa fitna wanajulikana , wameamua kupigilia

msumari Okwi asicheze kabisa. Wanajua

Simba haipati kitu lakini wanachotaka ni Simba

kutopoteza. ”

Juhudi za kumpata Okwi hazikuzaa matunda

kutokana na simu yake kupigwa zaidi ya mara

mbili bila ya majibu . Lakini memba mmoja wa

Friends of Simba kasisitiza kweli

walizungumza na Okwi lakini kwa lengo la

kumpa pole tu.

“Mimi si msemaji wa Friends of Simba, lakini

Okwi ni kijana wetu na tumezungumza naye

kumpa pole kutokana na matatizo ya fedha

anazodai na hajalipwa hadi leo , ubaya ni upi ?

“Msisahau, sisi ni ndugu zake na ndiyo

tulimleta Tanzania . Sasa hatuwezi kuwa

maadui, pia akipata matatizo tunaweza

kuzungumza naye au kumshauri tu,” alisema

akisisitiza kutoandikwa .

Mechi ya leo haiwezi kuzipa Yanga wala Simba

mabadiliko kwenye msimamo lakini ina nguvu

ya mechi ya watani , kila upande unataka

kushinda.

Wakati huohuo , Kocha Mkuu wa Yanga, Hans

van Der Pluijm, amefunguka na kusema

kamwe hafanyi kazi kwa kutegemea wachezaji

fulani wenye majina.

Van Der Pluijm amesema: “ Siku zote sifanyi

kazi kuangalia nani hayupo kikosini, labda

anaweza kutugharimu, nafanya kazi kwa

kuangalia nani ananifaa kikosini.

“Kazi yangu ni kuangalia kikosi nilichonacho

kinafanya vema kuelekea mchezo fulani , basi ,”

alisema kocha huyo wa zamani wa Feyenoord

ya Uholanzi .

Yanga itawavaa Simba leo bila nyota wengi,

wakiwemo Okwi mwenye mgomo baridi , Juma

Kaseja ( matatizo binafsi) , Juma Abdul (kadi

tatu za njano ) , Haruna Niyonzima, Said

Bahanuzi (wanaumwa) .


**Dida:Tambwe leo hapati goli ng'oo**

KIPA namba moja wa Yanga, Deogratius
Munishi ‘Dida ’, ameeleza kuwa katika mchezo
wa leo dhidi ya Simba, atahakikisha
mshambuliaji Amissi Tambwe hapati bao .
Mshambuliaji wa Simba, Amisi Tambwe.
Dida anatarajiwa kukaa langoni leo katika
mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu Bara msimu
huu dhidi ya watani wao wa jadi Simba kwenye
Uwanja wa Taifa jijini Dar .
Akizungumza na Championi Jumamosi , Dida
alisema atawapanga vizuri mabeki wake
kuhakikisha Tambwe hafungi bao lolote hata la
kuotea.
“Ninajua mchezo utakuwa mgumu lakini nina
imani mabeki wangu watanilinda vizuri na
kuhakikisha wanazuia kikamilifu mashambulizi
ya Simba na kutotoa nafasi kwa Tambwe
kufunga bao lolote .

No comments:

Post a Comment