Wednesday, April 16, 2014

Arsenal mwendo mdundo

West Ham ndio walioanza kufunga bao la kwanza,
kupitia kwa Matt Jarvis kunako dakika ya 40 ya
kipindi cha kwanza .
hata hivyo furaha ya West ham ilidumu kwa dakika
nne tu kwani hata kabla kivumbi hakijatua Lukas
Podolski aliisawazishia Arsenal na kuwapa the
gunners fursa ya kusitisha msururu wa matokeo
duni .
Ganga ganga ya mapumzikoni ilipelekea vijana wa
Arsene Wenger kufunga bao la pili na kuongoza kwa
mara ya kwanza katika mechi hiyo kupitia kwa
Olivier Giroud.
Masaibu ya West ham yalizidi Podolski alipofunga
bao la tatu na ushindi na kuisaidia Arsenal kuipiku
Everton katika nafasi ya nne katika jedwali la ligi
kuu ya Uingereza..
Hata hivyo Wenger atasubiri na kuomba Everton
ikunguwae dhidi ya Crystal palace katika mechi yao
itakayochezwa baadaye leo jioni.
Man City Inakungutana na Sunderland katika mechi
nyengine ya katikati ya wiki..

No comments:

Post a Comment