TIMU ya Soka ya Taifa ya Tanzania (Taifa
Stars), leo inaikabili Burundi (Intamba
Murugamba) katika mechi ya kimataifa ya
kirafiki kuadhimisha miaka 50 ya Muungano
wa Tanganyika na Zanzibar.
Tanganyika na Zanzibar ziliungana Aprili 26,
1964 na kuunda Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania chini ya waasisi Mwalimu Julius
Nyerere na Shekhe Amri Abeid Karume.
Burundi iliwasili nchini juzi tayari kwa mechi
hiyo itakayoanza saa 10 kamili kwenye Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam na kuchezeshwa na
mwamuzi kutoka Kenya, Anthony Ogwayo.
Taifa Stars imekuwa kambini jijini Dar es
Salaam tangu mwishoni mwa wiki iliyopita,
ikiwa inaundwa na wachezaji wazoefu pamoja
na vijana waliotokana na mchakato uliofanywa
katika mikoa mbalimbali.
Timu hii itawakosa wachezaji wake watatu
wanaocheza soka ya kulipwa ambao ni
Mbwana Samata, Thomas Ulimwengu
wanaochezea TP Mazembe na Mwinyi
Kazimoto anayecheza soka la kulipwa Qatar.
Aidha, mechi hiyo inatarajiwa kushuhudiwa na
kocha mpya wa Stars, Martinus Mart Nooij,
raia wa Uholanzi ambaye anatarajiwa
kuchukua nafasi ya Kim Poulsen aliyefukuzwa
na uongozi mpya wa soka Tanzania.
Akizungumzia mchezo huo, Ofisa Habari wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF),
Boniface Wambura aliwataka wananchi
kujitokeza kwa wingi ili kuwaona wachezaji
wapya waliopatikana katika mkakati wa
maalumu wa kupata wachezaji chipukizi wa
timu ya Taifa.
Wambura alisema wachezaji hao
watakaochanganyika na wachezaji wakongwe
wanatarajia kuonesha soka safi baada ya
kukaa kwa muda mrefu katika kambi maalumu
ya mafunzo.
Alisema ni mchezo wa aina yake hasa
ikizingatiwa kuwa timu hizo zote zipo katika
mchakato wa kujiandaa kushiriki kwenye
michuano ya awali ya Kombe la Mataifa ya
Afrika (Afcon).
Alisema ikumbukwe kuwa wachezaji hao
walicheza katika michuano ya Cecafa mwaka
jana ambapo Tanzania ilishinda kwa bao 1-0.
“Huu utakuwa ni mchezo wa aina yake kwa
kuwa wote wapo katika mchakato wa kunoa
vikosi kushiriki kwenye michuano hiyo
muhimu, hivyo basi wachezaji wanakuwa na
hali nzuri ya kimchezo katika kuhakikisha
kuwa wanacheza soka safi na lenge kuvutia,
watu waje kwa wingi kujionea soka hilo,”
alisema.
Wachezaji wa Stars waliopo kambini ni
Deogratias Munishi, Mwadini Ali, Aidan
Michael, Aggrey Morris, Erasto Nyoni, Hassan
Mwasapili, Kelvin Yondani, Said Morad, Amri
Kiemba, Frank Domayo, Himid Mao, Jonas
Mkude, Athanas Mdamu, Haruna Chanongo,
Juma Liuzio, Khamis Mcha, Mrisho Ngasa,
Ramadhan Singano na Simon Msuva.
Wengine ni Benedicto Mlekwa, Emma
Simwanda, Joram Mgeveje, Omari Kindamba,
Edward Mayunga, Shiraz Sozigwa, Yusuf
Mlipili, Said Ally, Abubakar Mohamed, Hashim
Magona, Omari Nyenje, Chunga Zito,
Mohammed Saidi, Ayoub Lipati, Abdulrahman
Ally na Paul Bundara.
Viingilio vya mechi hiyo ni VIP A Sh 20,000,
VIP B na C ni Sh 10,000 na cha chini ni Sh
5,000.
Friday, April 25, 2014
Stars kuminyana na Burundi leo.
MECHI ZA LEO
RATIBA YA SOKA LEO JUMAMOSI 26th April 2014:
*Barclays Premier League
2:45 PM - Southampton vs Everton
5:00 PM - Fulham vs Hull City
5:00 PM - Stoke City vs Tottenham Hotspur
5:00 PM - Swansea City vs Aston Villa
5:00 PM - West Bromwich Albion vs West Ham
United
7:30 PM - Manchester United vs Norwich City
*Spanish Primera División
5:00 PM - Granada vs Rayo Vallecano
7:00 PM - Getafe vs Malaga
9:00 PM - Real Madrid vs Osasuna
11:00 PM - Real Betis vs Real Sociedad
*Italian Serie A
7:00 PM - Bologna vs Fiorentina
9:45 PM - Internazionale vs Napoli
*German Bundesliga
4:30 PM - Bayern Munich vs Werder Bremen
4:30 PM - Hertha Berlin vs TSV Eintracht
Braunschweig
4:30 PM - Mainz vs Nurnberg
4:30 PM - TSG Hoffenheim vs Eintracht Frankfurt
4:30 PM - VfL Wolfsburg vs SC Freiburg
7:30 PM - Bayer Leverkusen vs Borussia
Dortmund
*French Ligue 1
6:00 PM - AC Ajaccio vs AS Monaco
9:00 PM - Evian Thonon Gaillard vs St Etienne
9:00 PM - Guingamp vs Valenciennes
9:00 PM - Montpellier vs Toulouse
9:00 PM - Nice vs Stade de Reims
9:00 PM - Stade Rennes vs Lorient
# EAT
Thursday, April 24, 2014
aongezewa mkataba tena au ndio wanamwondoa kimya kimya?
Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko
Logarusic amesema amekubaliana
na Zacharia Hanspope na huenda
akabaki Simba.
Logarusic amesema amekutana na
Hanspope ambaye ni Mwenyekiti wa
Kamati ya Usajili ya Simba na
wamezungumza na kukubaliana.
“Nitabaki Simba kwa makubaliano
yetu hasa kama yatatekelezwa,
nimezungumza na Hanspope,
tumekubaliana.
“Lakini nalazimika kurudi nyumbani
kwanza, nitaondoka kesho asubuhi
kwenda Croatia na baada ya hapo
nitasubiri makubaliano yetu,”
alisema Logarusic.
Alipoulizwa walichokubaliana na
Hanspope ambaye imeelezwa
anatarajia kugombea uenyekiti,
alisema.
“Tumezungumza mambo mengi,
lakini vizuri mkawasiliana naye na
kujua tulichokubaliana. Yeye ndiye
anaweza kuzungumza,” alisema,
kocha wa zamani wa Gor Mahia ya
Kenya.
Mkataba wake ulikuwa ni wa miezi
sita tu baada ya kuichukua Simba
katika mzunguko wa pili.
Pamoja na kuiwezesha kuitwanga
Yanga katika mechi ya Nani Mtani
Jembe, Logarusic alishindwa
kutamba kwenye Ligi Kuu Bara na
kumaliza katika nafasi ya nne.
klopp awagomea MANCHESTER UNTD
kocha wa dortimund kloop amekemea vikali dondoo za waandishi wa habari wa uingereza kwa uvumi wao wa yy kujiunga na manchester untd .. na amesema hana mpango huo... mkataba wake unaisha 2018 kwa sasa.
je hataki au kiti cha moto?
moyes kutua hapa
spur waonyesha nia ya kumtaka moyes.. baada ya kutemwa na club ya manchester united ...
Daniel Levy ambae ndio boss wa spurs anaonekana kuwa mpenzi mzur wa moyes.
##dlx
Wednesday, April 23, 2014
KUTOKA MAJUU: FC Barcelona appeal granted suspensive effect. Source fifa.com
The club FC Barcelona has lodged an appeal before the FIFA Appeal Committee against the decision of the FIFA Disciplinary Committee that sanctioned the club for breaches relating to the international transfer and registration of players under the age of 18. Together with the appeal, the club requested that its appeal be granted suspensive effect.
In this respect, the chairman of the FIFA Appeal Committee, Larry Mussenden, took into consideration the sanctions imposed against the club, the complexity of the matter, the start date of the next registration period – 1 July 2014 – and the fact that the FIFA Appeal Committee does not seem in a position to take a decision on the main issue early enough so that an eventual appeal of the club against its decision before the Court of Arbitration for Sport would still be decided before the beginning of the next registration period. Consequently, the chairman of the FIFA Appeal Committee considered that the appeal lodged by the club is to be granted suspensive effect.
In view of the foregoing, the chairman of the FIFA Appeal Committee assures that proper and adequate appeal proceedings will take place and, at the same time, that all rights of the club will be respected.
Tuesday, April 22, 2014
KUTOKA VYOMBO VYA HABARI VYA NJE: Man Utd begin hunt but Giggs not in race. Source BBC
Giggs, 40, has been put in temporary charge after
Moyes was sacked following just 10 months in the
job.
But the Premier League club feel an experienced
manager is needed to turn things round after this
season's slump.
Gary Lineker thinks United are "in crisis" after their
worst season since the Premier League began.
"They have not qualified for the Champions League
and are in a worse situation than 12 months ago,"
said the BBC Match of the Day presenter and
former England captain.
"Then they had lost their manager. This time they
don't even know whether they are going to be in
European football next season."
Former Manchester United captain Roy Keane,
speaking to ITV Sport, said Moyes should have
been given more time and accused the players of
letting the manager down.
"Some of the players should be ashamed of
themselves," he said.
"To be seventh is disappointing - and he will take
responsibility for that - but I don't think he's had
that support he needed and he deserved more
time."
Chelsea boss Jose Mourinho, talking before the
club's Champions League semi-final first-leg at
Atletico Madrid, added: "I just feel sorry for David,
like I feel sorry for every manager that loses his
job."
Moyes took over in July 2013 following the
retirement of Sir Alex Ferguson, who won 38
trophies, including 13 league titles and two
Champions League crowns, in a 26-year reign,
Robbie Savage, who was in the United youth ranks
with Giggs and was also a team-mate with Wales,
says the club need an experienced head as they
look to rebuild their squad over the summer.
"In the future, Ryan can be a successful manager,"
Savage told BBC Sport. "But going forward it's such
a huge transfer window for United that they need an
experienced man at the helm.
"Keeping Ryan as assistant manager would be a
great idea. He has United in his blood and has won
countless trophies.
"He would be able to learn the ropes from a
manager who has won trophies and been there and
done it."
Giggs, the most decorated player in English football,
has yet to decide whether to continue his playing
career.
After winning 13 Premier League titles and the
Champions League twice with United, as well as the
FA Cup four times and the League Cup three times,
his current contract runs out at the end of the
season.
It is understood United's hierarchy reached their
decision to dispense with Moyes reluctantly but
also in the knowledge they had little alternative.
They were forced to bring forward a public
announcement when British newspapers began
reporting the 50-year-old Scot's tenure was set to
end.
Sunday's 2-0 defeat at Everton means United,
currently seventh in the Premier League, will miss
out on the Champions League for the first time in 18
years.
It would also now take a favourable sequence of
results for them to secure a place in the Europa
League.
Poor results are not the only factor to count against
Moyes, who was sacked a year to the day after
United were crowned champions.
United officials hope Giggs will be able to restore a
sense of bullishness to the club, as well as a return
to the positivity and attacking philosophy for which
the club are so well known.
As the search for a second manager in less than a
year begins, Jurgen Klopp and Pep Guardiola
appear to be out of reach.
Klopp says his contract with Borussia Dortmund is
"unbreakable", while Guardiola has guided Bayern
to the Bundesliga title and Champions League
semi-finals in his first season in charge.
It leaves Netherlands coach Louis van Gaal in a
strong position, given Carlo Ancelotti is under
contract at Real Madrid and both Diego Simeone
and former United defender Laurent Blanc,
presently at Atletico Madrid and Paris St-Germain
respectively, have never coached in England.
Van Gaal's managerial curriculum vitae is
impressive.
The 62-year-old won three Dutch titles with Ajax
between 1991-97, as well as the 1995 Champions
League. He then secured two La Liga crowns at
Barcelona and enjoyed Bundesliga success at
Bayern Munich in 2010.
Savage believes he would be the perfect fit for
United and has a great relationship with striker
Robin van Persie.
"If Manchester United don't invest heavily in the
next transfer window, then they will go backwards,"
added the former Leicester City, Birmingham City,
Blackburn Rovers and Derby County midfielder.
"Van Gaal is a fantastic manager who has been
there and done it and will command respect."
Former United goalkeeper Raimond van der Gouw
says Van Gaal has an impressive pedigree.
"He has proved he's a good manager," Van der
Gouw told BBC Radio 5 live. "He's a champion in
Holland, Germany and Spain. He can be a good
manager for United."
Van der Gouw also insisted Moyes was always
likely to find it hard making an impact at Old
Trafford.
"If you have to go to a big club like United, you need
experience," he said. "It's a big step to go from
Everton to Manchester United. It's a much bigger
club, much more responsibility."
Former Manchester United manager Wilf
McGuinness succeeded Sir Matt Busby in June
1969, taking over in similar circumstances to
Moyes when his predecessor moved upstairs.
McGuinness reached three cup semi-finals, but
failed to win any silverware and was sacked in
December 1970.
"Everybody hopes to go to clubs like Manchester
United and stay the rest of their lives, but
unfortunately it did not work out," he told Radio 5
live.
"I'm sorry to see him go. It was a tricky job, but
Manchester United must have success and win
things."
Asked if there were similarities with his own
situation at Manchester United, McGuinness added:
"That's right, but it didn't work and several others
found that out as well."
Despite United's current troubles, club officials
believe they can regain ground quickly. "Reports of
our demise have been greatly exaggerated," one
club source told BBC Sport.
The finance is certainly available to strengthen the
squad, as it would have been had Moyes remained
in charge. United are also convinced their absence
from the Champions League need not be too much
of a handicap in the recruitment process.
But Lineker believes the players need to improve
their attitude.
"There is no question the players let David Moyes
down," said the former Barcelona, Everton,
Tottenham and Leicester striker.
"I hear pretty much first-hand that some of the
players were pretty dismissive of the new regime.
That is poor professionalism.
"Some of them have probably made life quite
difficult for David Moyes."
KUTOKA VYOMBO VYA HABARI VYA NJE: Dortmund rule out Juergen Klopp exit. Source ESPN
United confirmed that Moyes’ reign had been brought to
an end on Tuesday morning, and there has been
speculation that Klopp -- who guided Dortmund to last
season’s Champions League final -- is among the top
candidates for the role.
However, on Saturday, in response to claims Barcelona
have shown interest, Klopp had dismissed the
suggestion he could leave Borussia, and BVB director of
communication Sascha Fligge has now ruled out any
prospect the 46-year-old could take charge at Old
Trafford.
“Juergen Klopp already dismissed rumours linking him
to Barcelona on our official homepage on Saturday,”
Fligge told ESPN FC.
The former FSV Mainz coach extended his contract until
2018 in October and Fligge said there was no possibility
he would leave before then.
Before extending his deal, Klopp had been touted as a
potential successor to Sir Alex Ferguson, and Fligge
added: “We’ve already had this last year, but it’s final,
even if some people don’t want to believe it.”
Klopp, who guided Dortmund to a fourth consecutive
Champions League appearance at the weekend for the
first time in the club’s history, had said he was “still a bit
in love” with BVB when rejecting the Barca speculation.
Later on Tuesday morning, Klopp told The
Guardian: “Man Utd is a great club and I feel very
familiar with their wonderful fans, but my commitment to
Borussia Dortmund and the people is not breakable.”
KUTOKA VYOMBA VYA HABARI VYA NJE: United make move for Louis van Gaal. Source ESPN
Manchester United have already made the first steps
towards bringing Louis van Gaal in to replace sacked
manager David Moyes, Old Trafford sources have told
ESPN FC.
• Podcast: Chosen One? Sacked?
• Vote on Moyes' replacement at United
Having confirmed that Ryan Giggs will take temporary
charge on Tuesday morning, United are prepared to
keep an open mind about their next permanent boss and
will investigate other high-profile options, but the
Dutchman’s availability and evident willingness have
ensured United moved to make contact.
Van Gaal, who leaves his post as Netherlands boss after
the World Cup this summer, is seen as the likeliest
successor, potentially as a medium-term option until
United can appoint one of the other alternatives they are
still considering at this point.
The 62-year-old had been expected to join Tottenham
Hotspur as recently as February, and ex-Netherlands
star Ruud Gullit later told the BBC he thought it was a
“done deal,” but White Hart Lane sources say Van Gaal
has become extremely cool on that prospect over the
last two months and his position has completely
changed -- perhaps because the Dutchman had been
informed the United post could become open to him.
That, however, will not stop last season's Premier
League champions pursuing other avenues and seeing
what progress could be made with potential candidates
such as Juergen Klopp. Chief executive Ed Woodward is
known to be a huge fan of the German, but Borussia
Dortmund have told ESPN FC he will not leave and the
manager himself also ruled out an exit. United may still
test the waters to see how firm those sentiments are.
Whatever happens, the process will be very different
from the appointment of Moyes, with Sir Alex Ferguson’s
role greatly reduced after this season's debacle.
United's owners, the Glazer family, will assume an
increased and more direct influence in a more
business-like process, following on from the active
interest they took in managerial performance since
United’s FA Cup defeat to Swansea City in January.
That was the first time the club’s hierarchy began to
contemplate sacking Moyes, with the Glazers previously
much more detached as a consequence of the idea the
former Everton manager would be a long-term
appointment.
According to ESPN FC sources, by Sunday’s 2-0 defeat
at Goodison Park, almost everyone of significance at the
club had turned against Moyes -- the playing staff,
many directors and a number of sponsors. The Glazers
also wanted to ensure that the inevitable sacking
happened long before the World Cup, in order to allow
proper time to plan.
Meanwhile, sources state Moyes is only ever likely to
get compensation amounting to one or two years' worth
of the six-year contract he signed last summer. One
point of negotiation as regards that deal was the failure
to qualify for the Champions League, or to reach any
other acceptable target.
Samata,Ulimwengu na Kazimoto, kuikosa mechi dhidi ya Uganda
WACHEZAJI watatu wa Tanzania wanaocheza
soka la kulipwa nje watakosa katika mechi ya
kirafiki kati ya Taifa Stars dhidi ya Burundi
itakayochezwa Jumamosi wiki hii kwenye
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari jana,
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania
(TFF), Boniface Wambura alisema wachezaji
hao ni Mbwana Samatta, Thomas Ulimwengu
wanaocheza TP Mazembe ya Congo na Mwinyi
Kazimoto anayekipiga Qatar.
“Tuliandika barua kuwaomba wachezaji hao,
lakini tunaona kuwa kama watakosa mechi hii
basi watashiriki katika mechi ya mchujo
kuwania Kombe la Mataifa la Afrika, lakini
katika mechi ijayo watacheza wale wa ndani,”
alisema Wambura.
Alisema mchezo huo wa Jumamosi utakuwa ni
sehemu ya kusherehekea miaka 50 ya
Muungano.
Katika mechi hiyo itashuhudiwa na kocha
mpya wa Taifa Stars, Martinus Ignatus Nooij
ambaye anatarajiwa kutua nchini Ijumaa, na
baada ya mechi atatambulishwa rasmi na Rais
wa TFF, Jamal Malinzi.
Nooij ni kocha wa St. George ya Ethiopia na
tayari alikwishasaini mkataba wa miaka miwili
kuifundisha Stars. Burundi ‘Intamba
Murugamba’ itatua nchini Ijumaa tayari kwa
mechi hiyo itakayoshirikisha wachezaji
waliochaguliwa kwenye programu maalumu ya
maboresho ya Stars na wale wakongwe.
Wambura alisema wachezaji 39 wako kwenye
kambi ya Kunduchi Beach, Dar es Salaam
wakijifua kwa ajili ya mechi hiyo na ile ya Mei
mwaka huu itakayochezwa mkoani Mbeya.
Wachezaji wa Taifa Stars waliopo kambini ni
Deogratias Munishi, Mwadini Ali, Aidan
Michael, Aggrey Morris, Erasto Nyoni, Hassan
Mwasapili, Kelvin Yondani, Said Morad, Amri
Kiemba, Frank Domayo, Himid Mao, Jonas
Mkude, Athanas Mdamu, Haruna Chanongo,
Juma Liuzio, Khamis Mcha, Mrisho Ngasa,
Ramadhan Singano na Simon Msuva.
Wengine ni Benedicto Mlekwa, Emma
Simwanda, Joram Mgeveje, Omari Kindamba,
Edward Mayunga, Shiraz Sozigwa, Yusuf
Mlipili, Said Ally, Abubakar Mohamed, Hashim
Magona, Omari Nyenje, Chunga Zito,
Mohammed Saidi, Ayoub Lipati, Abdurahman
Ally na Paul Bundara.
Alitaja viingilio vya mechi hiyo kuwa ni VIP A
Sh 20,000, VIP B na C ni Sh 10,000 na cha
chini ni Sh 5,000.
Moyes OUT!!!
KOCHA Mkuu wa Manchester United, David
Moyes amefutwa kazi, ikiwa ni miezi 10 tu
baada ya kumrithi Sir Aex Ferguson.
Alitimuliwa baada ya mkutano na Makamu
Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ed Woodward katika
uwanja wa mazoezi wa Carrington,
Manchester jana saa mbili asubuhi kwa saa za
Uingereza.
Moyes, 50, alichaguliwa na Ferguson kuwa
mtu wa kumrithi wakati alipostaafu baada ya
miaka 26 ya kuiongoza klabu hiyo ya Old
Trafford mwishoni mwa msimu uliopita.
Kocha mchezaji, Ryan Giggs anatarajiwa
kuiongoza United katika mechi ijayo ya
nyumbani dhidi ya Norwich City, Jumamosi
wiki hii.
Kocha Mholanzi Louis Van Gaal, kocha wa
Borussia Dortmund, Jurgen Klopp, wa Atletico
Madrid, Diego Simeone na yule wa Paris St-
Germain, Laurent Blanc tayari wanatajwa
katika kumrithi Moyes.
Hata hivyo, Klopp ambaye mapema msimu huu
alisaini mkataba mpya hadi mwaka 2018,
amelieleza gazeti la Guardian la Uingereza
kuwa atabaki Signal Iduna Park.
“Man Utd ni klabu kubwa na ninajisikia vizuri
na mashabiki wake wa kuvutia,” alisema
Klopp. “Lakini utiifu wangu kwa Borussia
Dortmund na watu wake hauwezi kuvunjika.”
Aidha, imefahamika kuwa makocha Steve
Round na Jimmy Lumsden pia wameachia
ngazi nafasi zao, lakini kocha wa makipa Chris
Woods na kocha wa timu ya kwanza, Phil
Neville watabaki hadi mwisho wa msimu.
United ilikataa kutoa maoni kuhusu taarifa za
magazeti ya Uingereza juzi kwamba Moyes
ambaye aliondoka Everton na kusaini mkataba
wa miaka sita na mabingwa hao wa Ligi Kuu
ya England, angefukuzwa kabla ya mwishoni
mwa msimu huu. Lakini taarifa ya klabu hiyo
jana ilisema, “tungependa kuweka
kumbukumbu sawa, kwa kutoa shukrani kwa
kujituma kwa bidii, ukweli na uadilifu aliouleta
wakati wa kutekeleza jukumu lake.”
United iliyo katika nafasi ya saba zikiwa
zimebaki mechi nne, imejihakikishia kupata
pointi chache katika Ligi Kuu baada ya
kutaabika hasa Old Trafford msimu huu. Chini
ya Moyes, alipoteza mechi sita nyumbani,
alifungwa na Swansea katika Kombe la FA
kwenye Uwanja wa Old Trafford, na ilishindwa
kuizuia Sunderland kuwatoa katika nusu fainali
ya Kombe la Ligi.
Machi mwaka huu, baadhi ya mashabiki
walikodi ndege na kuruka juu ya uwanja huo
wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu dhidi ya
Aston Villa, ikiwa na bango lenye maneno
“Wrong One – Moyes Out” (ikimaanisha
Moyes hakuwa chaguo sahihi na anastahili
kuondoka) – ikiwa ni kama kupingana na
bango jingine uwanjani hapo lililombatiza
Moyes kuwa “Chosen One.”
Mashetani Wekundu hao pia watakosa
kucheza Ligi ya Mabingwa kwa mara ya
kwanza tangu mwaka 1995 na wako katika
hatari ya kukosa kabisa michuano ya Ulaya
kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1990.
United ilifuzu kwa robo fainali ya Ligi ya
Mabingwa kabla ya kutolewa na Bayern
Munich na Moyes alidai kuwa kikosi hicho
kilicheza vyema katika michuano hiyo.
Hata hivyo, kumekuwapo na madai kuwa
alikuwa hakubaliki kwa wachezaji wa Man
United, kiasi kwamba kiungo Anderson
alipohamia Fiorentina kwa mkopo Januari,
alidai wachezaji wa timu hiyo wanataka Moyes
aondoke. Baadaye alikanusha kauli hiyo.
Lakini Rio Ferdinand na Robin van Persie pia
wamewahi kukaririwa wakitoa kauli kama hizo,
wakati Javier Hernandez na Wilfried Zaha
wamewahi kuandika katika mitandao ya
Twitter kumkana kocha wao.
Baada ya kipigo Jumapili wiki hii dhidi ya timu
yake ya zamani Everton, ilikuwa dhahiri Moyes
siku zake katika Old Trafford zilikuwa
zinahesabika.
Alijiunga na timu hiyo baada ya misimu 11
katika Everton na alisema asingeweza kukataa
fursa ya kuhamia Old Trafford. Alianza kazi
rasmi Julai mosi.
Anakuwa kocha wa tatu kukaa muda mfupi
katika United, na ni mara ya kwanza tangu
Novemba 6, 1986 kwamba Manchester United
imefukuza kocha.
Moyes, ambaye ni raia wa Scotland,
ameifundisha United mechi 49, akimpiku Walter
Crickmer katika mechi 43 katika kipindi chake
cha kwanza kati ya viwili vya ukocha, wakati
Lal Hilditch ndiye aliyekaa muda mfupi zaidi,
akidumu kwa mechi 33 kati ya Oktoba 1926 na
Aprili 1927.
Friends of Simba wamzuia tambwe kwenda Yanga
Tambwe, ambaye hivi karibuni alihusishwa
kutaka kuikimbia klabu hiyo na kwenda
kujiunga na timu nyingine za ligi kuu , amepigwa
pini na klabu hiyo baada ya kuhakikishiwa
neema msimu ujao .
Mshambuliaji wa Simba, Amisi Tambwe.
Tambwe ambaye ni raia ya Burundi na ambaye
ndiye amekuwa msaada mkubwa wa timu hiyo
msimu huu baada ya kuifungia mabao 19
kweney ligi, amekuwa akihusishwa na taarifa
za kujiunga na Yanga na Azam FC lakini
ameelezwa kuwa kuna kundi moja , Championi
inafahamu kuwa ni Friends of Simba , linaweza
kuingia madarakani na kumtimizia mahitaji
yake yote .
Mwenyekiti wa Simba, Mhe; Ismail Aden Rage .
Akizungumza na Championi Jumatano ,
Tambwe alisema kuwa hivi karibuni uongozi
wa klabu hiyo umemtaka atulie na asiwe na
haraka za kutaka kuondoka katika kikosi hicho ,
kwani mambo mazuri yanakuja .
Alisema katika mazungumzo aliyofanya hivi
karibuni na Katibu Mkuu wa Simba , Ezekiel
Kamwaga, alimhakikishia kuwa mambo yake
yatakwenda sawa bila tatizo lolote hivyo
anatakiwa kuvumilia mpaka uchaguzi mkuu wa
klabu hiyo utakapomalizika na viongozi wapya
wakipatikana .
“Aliniambia hata kama nikiwa nyumbani
Burundi atakuwa akinijulisha kila kitu
kitakavyokuwa kinaendelea huku , hivyo nisiwe
na wasiwasi mambo yangu yatashughulikiwa,
kwani anaamini uongozi utakaoingia
madarakani, utakuja na mikakati mizuri zaidi
kwa kuwa anaamini wengi wao ni watu wenye
fedha .
“Kutokana na hali hiyo kwa sasa siwezi sema
kama nitaondoka Simba au nitabakia lakini kila
kitu kitajulikana hapo baadaye , acha
niwasikilizie kwanza viongozi hao , nimeelezwa
na mtu mwingine kuwa kuna kundi moja
linatwa Friends lina watu wenye uwezo sana
linaitaka timu nafikiri ni watu ambao
tutawezana,” alisema Tambwe ambaye
mkataba wake wa kuitumikia klabu hiyo
unamalizika mwakani .
Simba na Yanga wapigana vikumbo kumsajili kipa wa mtibwa.
SIMBA na Yanga zimeingia kwenye vita moja
ya usajili kwa mara nyingine baada ya kila
mmoja kuhitaji huduma ya kipa wa Mtibwa
Sugar, Hussein Shariff ‘Casillas’, kwa ajili ya
kuvitumikia vikosi vyao kwenye msimu ujao wa
ligi.
Vuguvugu hilo la usajili wa kipa huyo linakuja
baada ya timu zote mbili kuwa na matarajio ya
kupoteza makipa wao, hivyo kila timu inahaha
kutafuta wa kuziba pengo litakaloachwa wazi.
Mtu wa karibu na uongozi wa Simba alilieleza
Championi Jumatano habari hizo kwamba
mpaka sasa kipa aliye kwenye mahesabu ya
miamba yote hiyo miwili nchini ni kipa huyo
ambaye ameonyesha kiwango cha juu msimu
huu .
Chanzo hicho kilisema kwamba Yanga
itampoteza kipa wao, Ally Mustapha ‘Barthez’ ,
baada ya kuugomea uongozi kusaini mkataba
mpya huku Simba ikimpoteza Yaw Berko
ambaye kanuni mpya ya usajili inamtaka
kuondoka nchini kwa kuwa siyo raia wa nchi
hii.
“Berko hataweza kuongezewa mkataba Simba
kutokana na hali ya sheria mpya jinsi ilivyo na
huku Yanga pia Barthez kaugomea uongozi
kusaini mkataba mpya kutokana na vile
alivyosakamwa baada ya mechi ya 3 - 3 na
Simba, kwa hiyo hapo kila timu inahitaji mtu wa
kuziba pengo na ndipo kila mmoja akalitaja jina
la Casillas.
“Lakini sasa hii vita ipo chinichini kwa sababu
Simba hawajui kama Yanga inamtaka Casillas
wala Yanga pia hawajui kama Simba nao
wanamtaka kipa huyo , kwa hiyo kila mmoja
anapita njia yake kuangalia uwezekano wa
kumnasa, ” kilisema chanzo hicho .
Saturday, April 19, 2014
KUELEKEA BIG MATCH:SIMBA VS YANGA.updates zote click hapa
**Mzungu wa Yanga atinga mazoezini na jezi Nyekundu**
KATIKA hali ya kustaajabisha, Kocha Mkuu wa
Yanga, Hans van Der Pluijm, juzi alileta
sintofahamu baada ya kutinga mazoezini na
jezi yenye logo ya doti jekundu, ambayo ni
‘nuksi ’ Jangwani.
Mazoezi hayo yalifanyika kwenye Uwanja wa
Ununio, wakijifua kwa ajili ya mtanange wa
heshima dhidi ya watani wao Simba,
utakaopigwa leo kwenye uwanja wa Taifa Dar .
Mholanzi huyo alikuwa ametinga ‘full ’ jezi
nyeusi ya Klabu ya Feyenoord Rotterdam ya
nchini Uholanzi , inayotumia logo yenye doti
jekundu na nyeupe, ambayo ni kinyume na
miiko ya Yanga .
Ikumbukwe kuwa Yanga waliingia katika
mgogoro mkubwa na wadhamini wa Ligi Kuu
Bara, kampuni ya Vodacom , wakikataa kutumia
logo yenye doti jekundu kwa kile kilichoelezwa
na Baraza la Wazee kupitia katibu wao, Ibrahim
Akilimali, kuwa ni nuksi na kuongeza kuwa
katiba yao imeeleza kukataa rangi nyekundu
Jangwani.
Championi ilikuwa shuhuda katika mazoezi ya
Yanga, ambapo Mholanzi huyo hakuonekana
kujali, pengine hofu ikatawala labda wazee
hawajampa utaratibu na miiko ya klabu hiyo .
Feyenoord, ni moja ya timu zenye jina kubwa
nchini Uholanzi , ambayo mastaa wakubwa
akiwemo straika wa Manchester United , Robin
Van Persie, walipitia.
**CCTV kufungwa uwanjani**
KATIKA kuhakikisha ulinzi na usalama
unapatikana katika mechi ya leo Jumamosi kati
ya Yanga na Simba kwenye Uwanja wa Taifa,
jumla ya askari 400 wameandaliwa kwa ajili ya
kuweka usalama huku kukiwa na magari
mawili ya wagonjwa, yaani wale ambao
watazimia au kupata matatizo uwanjani hapo.
Mchezo huo wa watani wa jadi utapigwa leo
katika Uwanja wa Taifa ukiwa ni moja ya mechi
za kufungia msimu wa 2013/ 2014 ambapo
katika mchezo huo , mshindi wa pili ambaye ni
Yanga atakabidhiwa zawadi ya medali .
Akizungumza na Championi Jumamosi ,
Mtendaji wa Bodi ya Ligi , Silas Mwakibinga,
alisema wameandaa askari 400 na ‘Ambulance ’
mbili kwa ajili ya mchezo wa Simba na Yanga
huku ulinzi na usalama ukiwa wa hali ya juu .
Mwakibinga alisema kuwa wamejiandaa vyema
kabisa na michezo ya kufunga ligi kuu ambayo
yote itachezwa kesho katika viwanja
mbalimbali huku bingwa na mshindi wa pili
wakikabidhiwa zawadi zao kesho.
“Tumeandaa askari 400 kwa ajili ya usalama
katika mechi ya Simba na Yanga na ulinzi kwa
jumla umeimarishwa kila kona huku magari ya
kubebea wagonjwa tumeandaa mawili kwa
lolote litakalojitokeza .
“Kwa upande wa watu wa uwanja, wao
wamefunga ‘security ‘ kamera ( CCTV ) pale kwa
usalama zaidi na hiyo ni ya moja kwa moja si
kwa mchezo pekee wa kesho ( leo) , hivyo kila
kitu kinakwenda safi .
“Lakini kwa bingwa , atakabidhiwa zawadi yake
Chamazi ambazo ni kombe na medali za
dhahabu huku mshindi wa pili taifa yeye
atapewa medali zake pia ,” alisema
Mwakibinga.
**Friends of simba wamteka Okwi**
SAA chache kabla ya mechi ya watani , Yanga
dhidi ya Simba, kama kawaida vituko vinazidi
kuongezeka na mshambuliaji Emmanuel Okwi
anazidi kuwa tatizo .
Okwi alikuwa acheze mechi ya leo , akasusa
kwa kuwa anawadai Yanga dola 40,000 (Sh
milioni 64 ), lakini sasa Friends of Simba
wameingilia na kumteka mawazo zaidi kuwa
hana haja ya kucheza mechi ya leo ,
ataangushiwa mzigo wakipoteza.
Rafiki wa karibu wa Okwi amesema mara
nyingi mchezaji huyo amekuwa akijichimbia
katika hoteli anayoishi na hivi karibuni
alizungumza na memba wa kundi la Friends of
Simba linaloaminika kwa mipango ya kisoka na
kupewa ushauri kwamba hana sababu ya
kucheza mechi hiyo.
“Awali Okwi alikuwa apewe dola 20,000
ambazo ni nusu ya zile anazodai ili acheze ,
lakini baadaye mambo yakabadilika, ninafikiri
ametekwa mawazo na wale Friends of Simba.
“Unajua Friends wamerudi Simba, wanataka
kukiimarisha kikosi chao na ndiyo wametoa
msaada kuipeleka Simba Zanzibar na mmoja
wa mabosi wao ( Zacharia) Hans Pope ndiye
amelipa mshahara wa wachezaji wote maana
waligoma,” kilieleza chanzo kutoka Yanga .
“Kwa fitna wanajulikana , wameamua kupigilia
msumari Okwi asicheze kabisa. Wanajua
Simba haipati kitu lakini wanachotaka ni Simba
kutopoteza. ”
Juhudi za kumpata Okwi hazikuzaa matunda
kutokana na simu yake kupigwa zaidi ya mara
mbili bila ya majibu . Lakini memba mmoja wa
Friends of Simba kasisitiza kweli
walizungumza na Okwi lakini kwa lengo la
kumpa pole tu.
“Mimi si msemaji wa Friends of Simba, lakini
Okwi ni kijana wetu na tumezungumza naye
kumpa pole kutokana na matatizo ya fedha
anazodai na hajalipwa hadi leo , ubaya ni upi ?
“Msisahau, sisi ni ndugu zake na ndiyo
tulimleta Tanzania . Sasa hatuwezi kuwa
maadui, pia akipata matatizo tunaweza
kuzungumza naye au kumshauri tu,” alisema
akisisitiza kutoandikwa .
Mechi ya leo haiwezi kuzipa Yanga wala Simba
mabadiliko kwenye msimamo lakini ina nguvu
ya mechi ya watani , kila upande unataka
kushinda.
Wakati huohuo , Kocha Mkuu wa Yanga, Hans
van Der Pluijm, amefunguka na kusema
kamwe hafanyi kazi kwa kutegemea wachezaji
fulani wenye majina.
Van Der Pluijm amesema: “ Siku zote sifanyi
kazi kuangalia nani hayupo kikosini, labda
anaweza kutugharimu, nafanya kazi kwa
kuangalia nani ananifaa kikosini.
“Kazi yangu ni kuangalia kikosi nilichonacho
kinafanya vema kuelekea mchezo fulani , basi ,”
alisema kocha huyo wa zamani wa Feyenoord
ya Uholanzi .
Yanga itawavaa Simba leo bila nyota wengi,
wakiwemo Okwi mwenye mgomo baridi , Juma
Kaseja ( matatizo binafsi) , Juma Abdul (kadi
tatu za njano ) , Haruna Niyonzima, Said
Bahanuzi (wanaumwa) .
**Dida:Tambwe leo hapati goli ng'oo**
KIPA namba moja wa Yanga, Deogratius
Munishi ‘Dida ’, ameeleza kuwa katika mchezo
wa leo dhidi ya Simba, atahakikisha
mshambuliaji Amissi Tambwe hapati bao .
Mshambuliaji wa Simba, Amisi Tambwe.
Dida anatarajiwa kukaa langoni leo katika
mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu Bara msimu
huu dhidi ya watani wao wa jadi Simba kwenye
Uwanja wa Taifa jijini Dar .
Akizungumza na Championi Jumamosi , Dida
alisema atawapanga vizuri mabeki wake
kuhakikisha Tambwe hafungi bao lolote hata la
kuotea.
“Ninajua mchezo utakuwa mgumu lakini nina
imani mabeki wangu watanilinda vizuri na
kuhakikisha wanazuia kikamilifu mashambulizi
ya Simba na kutotoa nafasi kwa Tambwe
kufunga bao lolote .
Friday, April 18, 2014
DYLAN TOMBIDES FACTFILE. RIP
DYLAN TOMBIDES FACTFILE
March 8, 1994: Born in Perth, Australia.
2009: Joins West Ham aged 15.
2011: Diagnosed with testicular cancer.
September 2012: Makes West Ham debut.
April 18, 2014: Dies in London aged 20.
R.I.P
Pluijm:Tumejipanga kuiadabisha simba
KOCHA Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm,
amesema vijana wake wapo tayari kwa ajili ya
mchezo wa kesho dhidi ya wapinzani wao,
Simba na hana mchezaji yeyote aliyekuwa
majeruhi hadi sasa.
Yanga iliyoingia kambini juzi jioni kwenye Hoteli
ya Bahari Beach, Dar es Salaam ikiwa na
kikosi cha wachezaji 20, imepania kumaliza
msimu vizuri kwa kuifunga Simba ili kupoza
machungu ya kukosa ubingwa uliochukuliwa
na Azam FC katika dakika za mwisho.
“Nina uzoefu na michezo wa watani wa jadi,
huwa inakuwa migumu kwa kila timu kutokana
na kila timu kutaka kuonesha wapenzi,
mashabiki na wanachama wake kuwa wako
vizuri, Simba ni timu nzuri, lakini bado sioni
kikwazo cha kutuzuia tusiibuke na ushindi
katika mchezo huo,” alisema kocha huyo
Mholanzi.
Van Pluijm alisema vijana wake wanazidi
kuonesha mabadiliko makubwa kiuchezaji,
mafunzo yake wanaonekana kuyaelewa vizuri
hivyo kikubwa anaomba waendelee kuwa
katika hali nzuri kuelekea siku ya mchezo na
ana matumaini kitaibuka na ushindi kesho.
“Nina matumaini makubwa sana na wachezaji
waliopo kambini ambao kutokana na mbinu
nilizowapa wanaweza kuwafurahisha
mashabiki wa Yanga na kusahau baadhi ya
watu ambao watakosekana kwenye mchezo
huo,” alisema Van Pluijm.
Wachezaji 20 walioingia kambini kujiandaa na
mechi hiyo ya kesho dhidi ya mahasimu wao,
Simba ni makipa Deogratias Munish “Dida” na
Ally Mustafa “Barthez” kwa upande wa mabeki
ni Juma Abdul, Mbuyu Twite, Oscar Joshua,
Ibrahim Job, Rajab Zahir, Kelvin Yondani na
Nadir Haroub “Cannavaro.”
Viungo ni Frank Domayo, Hassan Dilunga,
Salum Telela, Hamis Thabit na Nizar Khalfani
wakati safu ya ushambuliaji wapo Didier
Kavumbagu, Mrisho Ngasa, Jerson Tegete,
Hamisi Kiza, Hussein Javu na Simon Msuva.
Kocha huyo alisema baada ya kushindwa
kutwaa ubingwa, lengo lake ni kuhakikisha
wanashinda mchezo huo ili kumaliza msimu
huu kwa kuwafunga watani zao Simba ambao
wamekuwa na wakati mgumu msimu huu
kutokana na kushika nafasi ya nne hadi saa.
Azam yatoa ofa,mashabiki wataingia BURE Azam complex kwenye mechi yake na jkt ruvu
UONGOZI wa mabingwa wapya wa soka
Tanzania Bara, Azam FC unatarajia
kutowalipisha kiingilio mashabiki katika
mchezo wa kesho dhidi ya JKT Ruvu kwenye
Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.
Katibu Mkuu wa timu hiyo, Nassor Idrissa
alisema sababu ya kufanya hivyo ni kuwapa
fursa mashabiki wao kuingia kwa wingi ili
kushuhudia timu yao ikikabidhiwa kombe la
ubingwa huo ambalo wanalitwaa kwa mara ya
kwanza tangu ilipopanda kucheza Ligi Kuu.
“Natarajia kukutana na viongozi wenzangu
halafu tuzungumze na Mwenyekiti wa Bodi ya
Ligi, Silas Mwakibinga tuone kama tunaweza
kuruhusiwa kuwaingiza mashabiki wetu bure
kwenye mchezo wetu wa mwisho dhidi ya JKT
Ruvu, ili washuhudie timu yao ikikabidhiwa
kombe,” alisema Idrissa.
Idrissa alisema kama yangekuwa mamlaka
yao wenyewe na siyo sheria za Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF), wangechukua uamuzi
wa moja kwa moja ya mashabiki kutolipa ili
kuwashukuru kwa sapoti waliyoipa timu yao
tangu mwanzoni mwa msimu hadi siku hiyo ya
mwisho ya kukabidhiwa kombe.
Kwa upande wake, Mwakibinga alisema
endapo Azam FC itataka mashabiki wasilipe
kesho, inatakiwa kukutana na Bodi yake na
kuzungumza ili kujua idadi ya mashabiki
watakaoingia na viingilio vyake.
“Sheria inawaruhusu Azam ila wanachotakiwa
kufanya ni kuja kuonana na viongozi wa Bodi
ya Ligi ili tujadiliane utaratibu tutakao tumia
ikiwemo kujua idadi ya mashabiki
watakaoingia na viingilio ambavyo
vimepangwa kwa ajili ya mchezo huo,” alisema
Mwakibinga.
Alisema lengo la kufanya hivyo ni kutaka
kufahamu idadi kamili ya tiketi ambazo
wataziandaa kwa mchezo huo na mapato
yatakayopatikana ili kufidia garama za
maandalizi zilizofanywa na Bodi hiyo.
Endapo hilo litafanikiwa, Azam FC watabidi
kuilipa Bodi ya Ligi zaidi ya Sh milioni 42
kutokana na kiingilio cha Sh 10,000 kwa
jukwaa kubwa ambalo lina uwezo wa kubeba
watazamaji 150 itaingiza Sh milioni 150 huku
majukwaa mengine ya mzunguko ambayo
kiingilio chake kwa kawaida huwa ni Sh 5,000,
itaingiza Sh 2,750,000. Uwanja una uwezo wa
kuchukua mashabiki 7,000.
J.K haipa tano Azam fc
RAIS Jakaya Kikwete amesema klabu ya Azam
FC inajitahidi katika uwekezaji wa soka kwa
vijana na kuitabiria kufika mbali katika soka
Afrika.
Kauli yake imekuja siku chache baada ya klabu
hiyo ya Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es
Salaam, kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara
kwa mara ya kwanza tangu ianzishwe mwaka
2007.
Rais Kikwete alisema hayo Ikulu, Dar es
Salaam juzi katika mahojiano maalumu na
kituo cha televisheni cha TBC1, mali ya Shirika
la Utangazaji Tanzania (TBC), yaliyohudhuriwa
pia na waandishi wa habari wa vyombo vingine
kuhusu miaka 50 ya Muungano.
Alisema hayo alipojibu swali la mwandishi
aliyetaka kujua maoni yake kuhusu maendeleo
ya michezo nchini.
“Tatizo letu ni menejimenti ya soka katika
klabu zetu. Mfano, Yanga na Simba
wangewekeza katika timu za watoto wa umri
mbalimbali na kuwa na utulivu, zingepiga hatua
kubwa,” alisema Rais Kikwete.
Alisema klabu inayojitahidi kuwekeza katika
soka nchini ni Azam, ambayo imewekeza kwa
vijana.
“Naamini Azam itakuwa timu kubwa Afrika kwa
sababu wana A,B,C za kuendeleza michezo,”
alisema.
Amesema klabu za Yanga na Simba, haziishiwi
na migogoro na migogoro hiyo imezorotesha
maendeleo ya soka nchini. Alisema timu hizo
maarufu nchini, zimekuwa zikipokezana
migogoro, yaani ukiisha Yanga, unahamia
Simba.
Rais Kikwete alisema Tanzania, watu
hawawekezi kwenye soka, bali wanawekeza
kwenye migogoro na mfano wa wanaowekeza
kwenye migogoro ni klabu za Yanga na Simba.
Rais Kikwete alisema kama Yanga na Simba,
zingekuwa na utulivu, zingewekeza kwa
wachezaji, ikiwemo kuendeleza timu za watoto
wa umri mbalimbali, hivyo kusonga mbele kwa
kasi. Mbali na soka, Rais alisema nchi
haijafanya vizuri katika riadha, netiboli, ngumi
na michezo mingine.
Alisema kila mara anapozungumzia suala la
michezo, suala hilo humpa uchungu. Alisema
tangu alipoingia madarakani, alijitahidi kusaidia
sekta hiyo, lakini bado haijawa na mafanikio.
Alisema katika hotuba yake ya mwaka 2005,
aliahidi mambo kadhaa, ikiwemo kuajiri kocha
wa timu ya taifa ya soka, na kweli alifanya
hivyo kwa kumuajiri Marcio Maximo.
“Niliwaambia kuwa miye nitaajiri kocha, nyie
mumhudumie kwa mahitaji mengine kama gari.
Nimefanya hivyo katika michezo mingine kama
netiboli, ngumi na riadha,” alifafanua Rais
Kikwete.
Alisema tatizo kubwa, lililopo katika sekta ya
michezo ni viongozi kushindwa kutimiza
mahitaji mengine ya makocha wa taifa, mfano
kuwapatia usafiri (magari).
Alilitaja tatizo jingine kubwa ni viongozi wa
michezo nchini, kushindwa kuwekeza kwenye
klabu zao, mfano kuwekeza kwa wachezaji.
Alisema timu za Ulaya zimepiga hatua kubwa,
kutokana na kuwekeza kwa wachezaji.
“Timu kubwa duniani kama Barcelona
zimewekeza kwa wachezaji hivyo na sisi
tuwekeze kwa wachezaji,” alisema rais.
Niyonzima: Ushindi lazima dhidi ya simba
KIUNGO wa kimataifa wa Rwanda anayecheza
Yanga, Haruna Niyonzima amesema hana
presha na kikosi kilichopo kwani ana uhakika
lazima kitoke na ushindi katika mechi dhidi ya
Simba itakayochezwa kesho kwenye Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam.
Niyonzima hajacheza mechi tatu za Ligi Kuu
dhidi ya Kagera Suger, JKT Ruvu, Oljoro JKT
na pia kuna uwezekano wa kutocheza mechi
hiyo dhidi ya Simba kutokana na kusumbuliwa
na homa ya matumbo.
Akizungumza na gazeti hili jana, Niyonzima
alisema kikosi kilichopo kina uwezo wa
kushinda mabao mengi, kwa vile wachezaji
wote ni wakali hata asipokuwapo yeye.
“Ninakiamini kikosi chetu ni kikali, hivyo
lazima tuondoke na ushindi, mimi sitakuwepo
lakini waliopo ni wazuri, watafanya vizuri, na
kuondoka na heshima,” alisema Niyonzima
anayejiuguza nyumbani kwake.
Alisema Simba wamekuwa wakijitapa kwa
maneno kila mwaka, lakini awamu hii Yanga
lazima wawashinde, kutokana na kikosi
kilichopo kucheza kwa kujiamini na juhudi
nyingi hivyo ni rahisi kushinda.
Akizungumzia afya yake, Niyonzima alisema
kwa sasa anaendelea vizuri na hali yake
imeimarika kiasi. Licha ya kuimarika hana
uhakika kama ataendelea kukipiga tena katika
msimu ujao.
“Kwa msimu ujao sifahamu, lakini tusubiri
tutajua, tuombe Mungu tumalize msimu huu
salama,” alisema Niyonzima.
Yanga na Simba zote hazitafuti nafasi ya
kushinda taji kwa sababu tayari bingwa
alishatangazwa toka wiki iliyopita ambao ni
Azam FC isipokuwa kila mmoja anasaka
heshima ili kupunguza utani.
Wakati huo huo, Msemaji wa Yanga, Baraka
Kizuguto alisema tayari wachezaji 20
wameingia kambini juzi kwenye Hoteli ya
Bahari Beach kwa ajili ya maandalizi ya mechi
hiyo ili kuja na nguvu ya kusaka ushindi.
Wednesday, April 16, 2014
Arsenal mwendo mdundo
West Ham ndio walioanza kufunga bao la kwanza,
kupitia kwa Matt Jarvis kunako dakika ya 40 ya
kipindi cha kwanza .
hata hivyo furaha ya West ham ilidumu kwa dakika
nne tu kwani hata kabla kivumbi hakijatua Lukas
Podolski aliisawazishia Arsenal na kuwapa the
gunners fursa ya kusitisha msururu wa matokeo
duni .
Ganga ganga ya mapumzikoni ilipelekea vijana wa
Arsene Wenger kufunga bao la pili na kuongoza kwa
mara ya kwanza katika mechi hiyo kupitia kwa
Olivier Giroud.
Masaibu ya West ham yalizidi Podolski alipofunga
bao la tatu na ushindi na kuisaidia Arsenal kuipiku
Everton katika nafasi ya nne katika jedwali la ligi
kuu ya Uingereza..
Hata hivyo Wenger atasubiri na kuomba Everton
ikunguwae dhidi ya Crystal palace katika mechi yao
itakayochezwa baadaye leo jioni.
Man City Inakungutana na Sunderland katika mechi
nyengine ya katikati ya wiki..
Saturday, April 12, 2014
Arsenal yatinga fainali kombe la FA.
Arsenal imefanikiwa kuingia fainali baada ya kushinda kwa penati 4-2 dhidi ya wigan hii ni baada ya kutoshana nguvu ya goli 1-1 katika dakika 90 za kwanza na dakika 30 za mda wa nyongeza .Je hii inaweza ikawa futa machozi ya washika bunduki hawa kuinua ndoo baada ya mda mrefu wa ukame???? mimi na wewe Tusubiri fainali.
Mabingwa wa kombe la dunia la watoto wa mtaani wazawadiwa fedha
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amewazawadia
washindi wa Kombe la Dunia la Watoto wa
Mitaani Sh 500,000 kila mchezaji, huku
akiwaongezea kidogo wachezaji watatu
waliong’ara nusu fainali na fainali.
Timu hiyo ya watoto wenye umri chini ya
miaka 16, ilipangwa Kundi la 2 pamoja na
Argentina, Nicaragua, Philippines na Burundi na
kulikuwa na makundi matatu.
Tanzania iliingia nusu fainali kwa kuwa mshindi
wa pili na pia kumenyana na Marekani na
kuichapa mabao 6-1 na baadaye kuitoa
Burundi kwa mabao 3-1.
Pinda alitangaza zawadi hiyo nyumbani kwake
mjini Dodoma jana, alipokutana na washindi
hao kwa chakula cha mchana na kuwapongeza
kwa kuitangaza Tanzania vyema.
“Mmetupa heshima kubwa sana na nimeona
tusiishie kwa kuwaona bali mpitie katika Bunge
Maalumu wajumbe watafurahi kuwaona.
Changamoto mliyotupa ni kubwa sana kwangu
binafsi, kwa viongozi na Wizara,” alisema
Waziri Mkuu Pinda.
Wachezaji walioongezewa kidogo zaidi ya Sh
500,000 ni Kipa Bora, Emmanuel Chaka,
aliyepewa kombe na mfungaji wa mabao
manne katika nusu fainali dhidi ya Marekani,
Michael Simon.
Mwingine aliyeongezewa zawadi ni mfungaji
wa mabao yote matatu ya fainali dhidi ya
Burundi, Frank Willium. Kabla ya kuanza
kuzungumza, Pinda alitoa nafasi kwa mmoja
wa watoto hao, Majuto Ismail, aeleze hali
ilivyokuwa katika michuano hiyo mpaka
wakafikia mafanikio hayo.
Majuto aliyecheza katika michuano iliyopita
Afrika Kusini na kuwa washindi wa pili na
katika michuano hii, alikwenda kama Meneja,
alisema walipofika Brazil katika Jiji la Rio de
Janeiro, walikuwa timu ya sita kufika.
Mashindano yalipoanza alisema walicheza kwa
kujituma na walikuwa na nidhamu nzuri kwa
kufuata sheria, kiasi ambacho kama
kungekuwa na zawadi ya nidhamu
wangepewa.
Baada ya kushinda, Majuto alisema
walikwenda kutembelea vivutio vya Brazil,
ikiwemo wanakoishi watoto wa mazingira
hatarishi.
Majuto aliyesema kuwa hapendi kuitwa mtoto
wa mitaani kwa kuwa mtaa hauzai, alitakiwa
na Pinda kufafanua hilo eneo walilokwenda
linafanana na eneo gani Tanzania, na akajibu
linafanana na Mwanza ambako yeye amekulia
katika mazingira magumu.
Akifafanua kuhusu dhana ya maisha ya watoto
wa mazingira magumu katika nchi
zilizoendelea na nchi masikini, Pinda alisema
hata jina Kombe la Dunia la Watoto wa Mitaani
halipendi, lakini ndivyo linavyoitwa.
Alifafanua kuwa watoto hao ni ambao
hawajakua katika mazingira nadhifu na kupata
mapenzi ya baba na mama. Alisema pamoja na
mazingira hayo, watoto hao wametoa funzo
kuwa hata katika mazingira magumu,
wameonesha karama zao na kuleta heshima
kwa Taifa na kazi iliyopo ni kukuza karama
zao.
“Msikate tamaa kwa kuitwa hivyo, inaonekana
kama vile tusi, lakini ni aina ya uhalisia ambao
mmeutumia kuleta kitu kizuri,” alisema Pinda
na kuongeza kuwa atawasiliana na uongozi wa
Mkoa wa Mwanza wawape mapokezi mazuri
na yeye akitembelea mkoa huo, atakwenda
kuwaona.
Katika hatua nyingine kabla ya kuonana na
Pinda, wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba
waliamua kuchangia timu hiyo ya watoto wa
mitaani.
Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la
Katiba, Samia Suluhu Hassan, alisema jana
wataandaa utaratibu kwa wajumbe wa Bunge
hilo wanaopenda kuwachangia watoto hao
kufanya hivyo.
Alisema hayo alipokuwa akijibu hoja ya
Mbunge wa Viti Maalumu, Diana Chilolo,
aliyeomba wajumbe wa Bunge Maalumu,
wawachangie watoto hao waliopeperusha
vyema Bendera ya Tanzania nchini Brazil.
Watoto hao walifika jana katika Bunge
Maalumu na kutambulishwa kuwa wageni wa
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo, Dk Fenella Mukangara.
Naye Naibu Waziri wa Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo, Juma Nkamia
alifananisha washindi hao na timu ya Mathare
United ya Kenya ambayo iliundwa na watoto
wa mitaani na baadaye kufanikiwa kuchukua
ubingwa wa Afrika Mashariki.
Alisema timu hiyo ilitunzwa na kutoa wachezaji
wazuri akiwemo Victor Wanyama ambaye leo
anacheza katika ligi kubwa duniani, Ligi Kuu ya
England katika klabu ya Southampton.
Katika hatua nyingine, Rais Jakaya Kikwete
ameipongeza timu ya Watoto wa Mitaani ya
Tanzania kwa kutwaa Kombe la Dunia jijini Rio
de Janeiro, Brazil.
“Mmetuwakilisha vyema, ninawapongeza
sana, pia mmewapa moyo watoto wengine
wote wenye vipaji maalumu, lakini
hawakubahatika kuwa na makazi rasmi,
hongereni sana,” alisema Rais Kikwete.
“Hongereni kwa kujituma na kucheza kwa
ustadi,” alisema Rais na kuwaasa watoto hao
“ongezeni bidii, nidhamu na mazoezi ya
kutosha na hakika mtafanikiwa zaidi na
kulibeba jina la Tanzania mbali zaidi ya hapa
katika ulimwengu wa soka duniani, kwani
hakuna kisichowezekana kama mtazingatia
maelekezo, mafunzo, bidii na nidhamu ya yote
mnayofanya.”
Matokeo yaleo EPL
Crystal Palace 1-0 Aston Villa
Fulham 1-0 Norwich City
Southampton 0-1 Cardiff City
Stoke City 1-0 Newcastle United
Sunderland 0-1 Everton
West Bromwich Albion 3-3 Tottenham
Hotspur
Friday, April 11, 2014
WENGER: Nina hasira na ushindi, sasa naenda kuchukua FA.
KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema
ni matumaini yake kuwa anaenda kumaliza kiu
ya kukosa ushindi kwa muda mrefu kwa
kutwaa Kombe la FA.
Wenger alisema ikiwa ni mwaka wa tisa sasa
bila ya kuchukua kombe, anaona kuwa msimu
huu ni muda mwafaka wa kuchukua kombe
hilo.
Alisema ana imani kuwa katika mchezo wake
wa leo wa nusu fainali dhidi ya Wigan, ushindi
ndio kupaumbele kikubwa na amekuwa
akisisitiza kwa kiasi kikubwa suala zima la
ushindi katika ligi hiyo.
Baada ya kutolewa kwenye kinyang'anyiro cha
kuwania Ligi ya Mabingwa Ulaya, sasa nia
yake kubwa ni kuhakikisha kuwa anachukua
moja kati ya mataji ya ndani.
“Ligi ya Mabingwa ndio ilikuwa kila kitu kwetu
na hadi sasa bado naumia kukosa ubingwa
huo, lakini kwa sasa mimi pamoja na timu
yangu nzima tunahamishia harakati zetu za
ushindi kwa michuano ya ndani,” alisema
Wenger ambaye amekuwapo Arsenal kwa
miaka 18 sasa.
“Najua kila mmoja aliyepo kwenye Ligi ya
England anakuwa na shauku ya kuhakikisha
kuwa anashinda na kuibuka na ushindi na ndio
azma yetu kwa sasa,” alisema Wenger.
“Usishangae kuona kwa miaka tisa sina kombe
lolote, sasa ndio ujue ni kwa kiasi gani
ninakuwa na hasira ya ushindi kwa sasa na
nipo tayari kuchukua Kombe la FA,” alisema
Wenger.
Alisema nia yao kwa sasa ni kushinda
mashindano na hasa ikizingatiwa kuwa
hawana mchakato wowote wa kuwania Ligi ya
Mabingwa Ulaya.
Aliongeza kuwa wanarejea Wembley wakiwa
wamejikamilisha na kusahau yote yalyotokea
kwenye Kombe la mwisho la FA, Arsenal
walichukua mwaka 2005 baada ya kuitoa
Manchester United katika fainali.
Mbeya city: hatujaongwa na azam ili tuhujumu mechi
TIMU ya soka ya Mbeya City ya hapa,
imekanusha tuhuma zinazotolewa dhidi yake
za kula njama za kuiwezesha Azam FC
kushinda katika mchezo wa kesho ili timu hiyo
inyakue ubingwa wa Tanzania bara.
Tuhuma zinazotajwa dhidi ya timu hiyo ni
kuahidiwa na Azam kununuliwa basi la kisasa
kwa ajili ya timu na pia Kocha Mkuu Juma
Mwambusi kununuliwa nyumba eneo la
Chamazi jijini Dar es Salaam ili apange kikosi
chenye wachezaji dhaifu siku ya mchezo.
Zipo tuhuma pia za wachezaji wa kikosi cha
kwanza kupewa rushwa ili siku ya mchezo huo
kwenye Uwanja wa Sokoine, wacheze chini ya
kiwango na kuipa ushindi Azam FC ili itangaze
ubingwa.
Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya
habari na Katibu wa Mbeya City, Emmanuel
Kimbe, imebainishwa kuwa tuhuma hizo si za
kweli na timu hiyo inaamini kuwa tuhuma
zinaibuliwa na watu wachache wasiopenda
mafanikio ya timu hiyo iliyobahatika kujizolea
mashabiki lukuki ndani na nje ya Mkoa wa
Mbeya tangu kutinga kwake Ligi Kuu ya
Tanzania Bara msimu huu.
Kimbe aliyezitaja tuhuma hizo sawa na
propaganda na upotoshaji, alisema mpango wa
Halmashauri ya Jiji la Mbeya kununua basi la
timu zake za soka na netiboli ambazo zote
ziko Ligi Kuu za michezo husika.
“Halmashauri ya jiji la Mbeya imekuwa katika
mchakato wa kutafuta na kununua basi kwa
ajili ya matumizi mbalimbali ya Halmashauri,
ikiwemo kutumiwa na timu zake (netiboli na
mpira wa miguu) ambazo zote zipo Ligi Kuu ya
michezo husika kwa kufuata sheria ya
manunuzi ya umma,” alisema Kimbe.
Alisema mchakato huo ulianza Agosti 8, 2013,
kwa kutangaza zabuni baada ya kutenga bajeti
katika mwaka wa fedha 2012/13 na 2013/14,
na kwamba hawakupata mzabuni mwenye
sifa, hivyo tangazo hilo lilirudiwa kutangazwa
tena Februari 12, mwak huu.
Alisema pamoja na mchakato huo, pia klabu
inaendelea na mazungumzo na wadau
mbalimbali wenye nia ya kuwekeza kwa
udhamini wa bidhaa zao, moja ya maeneo ya
udhamini ni ununuzi wa basi la wachezaji
taratibu na makubaliano haya
yatakapokamilika wapenzi wa soka
watajulishwa, hivyo tuhuma za kuahidiwa
kununuliwa basi, zinalenga kuidhalilisha timu
hiyo.
Kuhusu tuhuma kwa kocha Mwambusi
kununuliwa nyumba Chamazi ili apange kikosi
dhaifu kesho, Kimbe alisema kocha huyo ni
mwajiriwa wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya,
kwa maana hiyo ni mtumishi wa umma hivyo
amekuwa na timu hiyo kwa muda mrefu sasa
na ataendelea kuwepo.
Alisema kumekuwepo na maneno yasiyofaa
dhidi ya Mwambusi tangu mzunguko wa pili wa
ligi kuanza, aliyosema yamekuwa na nia ya
kuharibu mwenendo wa timu ili ianze kufanya
vibaya, lakini zaidi ya hapo yana nia ya
kumdhalilisha kocha na taaluma ya ukocha
nchini.
Katibu huyo aliwapongeza pia wachezaji wa
Mbeya City, akisema ndiyo wachezaji wenye
nidhamu kubwa katika ligi ya mwaka huu ndani
na nje ya uwanja, kwani ni waadilifu na
wanajua wanataka nini.
Mbeya City ambayo inashika nafasi ya tatu
katika msimamo wa Ligi Kuu, kesho
inaikaribisha Azam FC kwenye Uwanja wa
Sokoine katika mechi ambayo timu ya Chamazi
ikishinda, itatangazwa bingwa.
Wednesday, April 9, 2014
Logarusic (kocha wa simba) aipa nafasi azam kuchukua ubingwa
KOCHA wa Simba, Zdravko Logarusic
amesema Azam FC ishindwe yenyewe
kunyakua ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara,
kwa sababu ana uhakika wa kuifunga Yanga
kwenye mchezo wa mwisho wa ligi hiyo Aprili
19, mwaka huu.
Logarusic, ambaye kikosi chake hakina uwezo
hata wakumaliza ligi ya msimu huu kwenye
nafasi ya tatu, alisema anachotaka ni
kuendeleza rekodi yake ya kuifunga Yanga
kwa sababu ndiyo timu pekee yenye ushindani
na kikosi chake tofauti na Azam.
“Ni kweli hatuna uwezo hata wa kumaliza
nafasi ya tatu na hiyo ndiyo itakuwa mechi yetu
ya mwisho kwenye msimu, tumepanga
kuwavurugia Yanga kwa kuwafunga na
kuwapa furaha mashabiki wetu ambao msimu
huu umekuwa mbaya kwao,” alisema
Logarusic.
Kocha huyo raia wa Croatia, alisema pamoja
na upungufu uliopo kwenye kikosi chake
ukilinganisha na kile cha Yanga, hawatakubali
kufungwa na kuwafanya wapinzani wao
walipize kisasi cha mabao 3-1, ambacho
waliwapa kwenye mechi ya Mtani Jembe
Desemba 21, mwaka jana.
“Najua Yanga wana timu nzuri, lakini Azam ni
zaidi yao na ndiyo timu ninayoipa nafasi kubwa
ya kuchukua ubingwa kutokana na ukali wa
kikosi walichokuwa nacho ambacho sidhani
kama kinaweza kikafanya mzaha,” alisema
Logarusic.
Manchester united, Fc Barcelona watolewa UEFA
Machester united 1-3 Bayern Munich
Atletico Madrid 1-0 Barcolona
Yanga yachapa mtibwa bao 2-1
Young Africans imeendeleza wimbi lake la ushindi
katika michezo ya Ligi Kuu Tanzania bara hatua ya
lala salama baada ya kuichapa timu ya Wakata
miwa Kagera Sugar kutoka mjini Bukoba kwa
mabao 2-1 mchezo uliofanyika jioni ya leo kwenye
dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Ikiwa na kumbukumbu ya ushindi mnono wa mabao
5-1 mwishoni mwa wiki dhidi ya maafande wa jeshi
la Kujenga Taifa nchini JKT Ruvu, Kikosi cha Young
Africans kiliingia uwanjani kuhakikisha kinapata
pointi 3 jambo ambalo vijana walifanikiwa.
Kwa matokeo ya leo ya 2-1 dhidi ya Kagera Sugar
yanaipelekea Young Africans kufikisha pointi 52
ikiwa ni pointi moja nyuma ya Azam FC yenye pointi
53 na wauza ramba ramba wakiwa nyuma kwa
mchezo mmoja kufuatia mechi yao kuahirishwa leo
kutokana na mvua zilizopelekea uwanja wa
mabatini kujaa maji.
Hamisi Kizza aliipatia Young Africans bao la kwanza
dakika ya tatu ya mchezo akiunganisha krosi safi
ya winga Saimon Msuva aliyewatoka walinzi wa
Kagera Sugar na kumimina krosi hiyo iliyomkuta
mfungaji aliyeukwamisha mpira wavuni na kufikisha
idadi ya mabao 12 kwenye michezo wa Ligi Kuu
msimu huu.
Young Africans iliendelea kulishambulia lango la
Kagera Sugar kupitia kwa Didier Kavumbagu,
Saimon Msuva, Mrisho Ngasa na Hamisi Kizza lakin
kutokua makini kwa wachezaji hao kulifanya
waopoteze nafasi nyingi za wazi.
Dakika ya 34 ya mchezo, mshambuliaji wa
kimataifa kutoka nchini Burundi Didier Kavumbagu
aliwainua washabiki wa Young Africans vitini baada
ya kuipatia timu yake bao la pili baada ya jitihada
zake binafasi kufuatia kuwazidi ujanja walinzi wa
Kagera Sugar na kuukwamisha mpira wavuni na
kufikisha idadi ya mabao 11 kwenye VPL.
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza
zinamalizika, Young Africans 2 - 0 Kagera Sugar.
Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya
mabadiliko na kusaka mabao ya mapema, lakini
uimara wa mlinda mlango wa Yanga SC Deo Munish
"Dida" ulikua kikwazo kwa washambuliaji wa
Kagera Sugar na kuokoa michomo zaidi ya mitatu
ya hatari langoni mwake.
Makosa ya mlinzi wa Young Africans Oscar Joshua
yaliipatia Kagera Sugar bao la kwanza dakika ya 63
baada ya mpira wa kichwa aliomrudishia golikipa
wake Dida kunaswa na Daud Jumanne ambaye
aliukwamisha wavuni na kuhesabu bao la kwanza
kwa timu yake.
Young Africans iliendelea kulishambulia lango la
Kagera Sugar bila mafanikio kipindi cha pili kufuatia
washambuliaji wake kutokua makini katika
umaliziaji na kukuta mipira ikiokoloewa na golikipa
wa Agathony Anthony na mingine kuwa kona
ambazo hazikuzaa matunda.
Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Young
Africans 2- 1 Kagera Sugar.
Mara baada ya mchezo wa leo kikosi cha Young
Africans kesho kitaendelea na mazoezi jioni
kujiandaa na safari ya jijini Arusha kwenda kuwavaa
JKT Oljoro mwishoni mwa wiki kabla ya kurejea Dar
es salaam kumalizia mchezo wa mwisho dhidi ya
watani wa jadi Simba Sc.
Young Africans: 1.Deo Munish "Dida" 2. Jumva
Abdul, 3.Oscar Joshua, 4.Nadir Haroub
"Cannavaro", 5.Kelvin Yondani, 6.Frank Domayo,
7.Saimon Msuva, 8.Hassan Dilunga, 9.Didier
Kavumbagu, 10.Mrisho Ngasa/Hussein Javu,
11.Hamisi Kizza/Nizar Khalfani
MECHI YA AZAM VS RUVU YASOGEZWA
Mechi ya Azam FC dhidi ya Ruvu
iliyokuwa ilikuwa ichezwe leo kwenye
Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi,
imeahirishwa. mechi hiyo imeahirishwa kutokana na mvua kubwa iliyonyesha katika eneo hilo.
Taarifa kutoka Kamati ya Ligi zinaeleza
kuwa mvua kubwa na upepo
zimesababishwa kuahirishwa kwa mechi
hiyo.
Bado haijaelezwa kama itachezwa kesho au itapangiwa siku nyingine.
Tuesday, April 8, 2014
Tanzania bingwa Kombe la DUNIA watoto wa mtaani
TIMU ya soka ya Taifa ya Watoto wa Mitaani
ya Tanzania imetwaa ubingwa wa Kombe la
Dunia kwa Watoto wa Mitaani baada ya juzi
kuilaza Burundi mabao 3-1 katika mchezo wa
fainali uliochezwa jijini Rio de Janeiro, Brazil.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF) jana, mshambuliaji Frank
William alifunga mabao matatu katika mechi
hiyo iliyochezwa uwanja mkongwe na maarufu
wa klabu ya Fluminense huku mgeni rasmi
akiwa Waziri wa Fedha wa Uingereza, George
Osborne.
Tanzania ilipata tiketi ya kucheza fainali baada
ya kuitandika Marekani mabao 6-1 ambapo
hadi mapumziko ilikuwa mbele kwa mabao
4-0.
Burundi ilipata tiketi ya kucheza fainali baada
ya kuifunga Pakistan mabao 4-3 katika mechi
ya nusu fainali ya pili.
Timu ya Tanzania itarejea nchini keshokutwa
ambapo itatua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
wa Julius Nyerere (JNIA) saa 10 jioni kwa
ndege ya shirika la ndege la Muungano wa
Falme za Kiarabu, Emirates.
Monday, April 7, 2014
Sunday, April 6, 2014
Saturday, April 5, 2014
Friday, April 4, 2014
06-04 18:00 West Ham - Liverpool 07-04 22:00 Tottenham - Sunderland 05-04 17:00 Norwich - West Bromwich 05-04 17:00 Newcastle - Manchester United 05-04 14:45 Manchester City - Southampton 05-04 17:00 Hull - Swansea 06-04 15:30 Everton - Arsenal 05-04 19:30 Chelsea - Stoke 05-04 17:00 Cardiff - Crystal Palace 05-04 17:00 Aston Villa - Fulham
Nani kufuzu kuingia ligi kuu tanzania bara ??? Stand utd Vs Mwadui
HOMA ya michezo miwili ya Kundi C Ligi
Daraja la Kwanza Tanzania Bara itakayoamua
timu moja kati ya mbili za Mkoa wa Shinyanga
zinazochuana kuwania kushiriki katika Ligi Kuu
Tanzania Bara msimu ujao, Standa United na
Mwadui FC imezidi kupanda kuelekea mechi za
kesho.
Stand United na timu iliyoshuka daraja msimu
uliopita ya Toto African ya Mwanza zitakwaa
kwenye Uwanja wa CCM Kambarage mjini
hapa wakati pambano jingine litafanyika
kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma kati
ya Polisi Dodoma watakapoikaribisha Mwadui
FC.
Tambo na majigambo ya mashabiki wa timu
hizo mbili yametawala anga la Mkoa wa
Shinyanga kwa wapenzi kutambiana nani
ataibuka mshindi kesho ili kuingia Ligi Kuu
msimu ujao huku kila mmoja akitamba kuwa
timu yake itashinda kwa kishindo.
Kesho ni siku ya mwisho kwa michezo ya
Kundi C kwa timu zote nane kuteremka
dimbani kuwania pointi tatu muhimu huku
Mwadui ikiwa kileleni baada ya kujikusanyia
pointi 28 ikifuatiwa na ndugu zao wa Stand
United yenye pointi 26, Toto African ikiwa na
pointi 21 na JKT Kanembwa ya Kigoma wakiwa
na pointi 20.
Akizungumza na gazeti hili, mpenzi wa soka
mkoani hapa, Ally Nassoro wa Maganzo
alisema ana uhakika wa asilimia 100 kuwa
nafasi kubwa ya kuingia kwenye Ligi Kuu iko
kwa Mwadui kwa kuwa ina pointi 28 hata
ikitoka sare itafikisha pointi 29 na itakuwa na
nafasi kubwa zaidi ya kuizidi idadi ya mabao
Stand United ambayo ikishinda mchezo wake
dhidi ya Toto itafikisha pointi 29 sawa na
Mwadui.
Mpenzi mwingine, Ndimila Jilala wa Ngokolo
katika Manispaa ya Shinyanga alisema ushindi
wa Stand United uko dhahiri kwa kuwa pamoja
na ushindi kesho, bado inategemea rufaa yake
iliyokata Shirikisho la Soka (TFF), dhidi ya JKT
Kanembwa kwa kuwachezesha wachezaji
iliowasajili kwenye dirisha dogo kinyume cha
maelekezo ya TTF katika mchezo ambao
ilishinda bao 1-0.
Jilala alishangazwa na ukimya wa TFF
kuchelewesha kutoa maamuzi ya rufaa hiyo
mpaka sasa ligi inakaribia kufikia tamati, jambo
linalotia wasiwasi ni kwa nini rufaa hiyo
imechelewa kiasi hicho.
Timu nyingine za Kundi C ambazo tayari
zimepoteza matumaini ya kuingia Ligi Kuu
kutokana na uchache wa pointi ni Polisi
Tabora yenye pointi 17, Polisi Mara pointi 12,
Polisi Dodoma pointi 11 na Pamba pointi nane.
Beno Njovu:Hafukuzwi mchezaji
UONGOZI wa Yanga umesema hauna mpango
wa kuwatimua wachezaji wake wakati huu ligi
ikiwa inaendelea na zaidi inafikiria kwa vipi
itaimarisha kikosi chake kitetee ubingwa wa
Ligi Kuu Tanzania Bara.
Baada ya kumalizika kwa mechi kati ya Yanga
dhidi ya Mgambo JKT mwishoni mwa wiki
iliyopita, kumekuwa na uvumi wa kufukuzwa
kwa baadhi ya wachezaji waliovurunda katika
mchezo huo.
Katika mchezo huo, Yanga ilipata kipigo cha
mabao 2-1 katika mchezo uliofanyika kwenye
Uwanja wa CCM Mkwakwani, Tanga na hivyo
kutibua mbio zao za kutetea ubingwa na
kubaki katika nafasi ya pili ikiwa na pointi 46,
mashabiki wake wakiwa na hofu kutochukua
taji baada ya kukimbizwa kwa pointi na Azam.
Akizungumza na gazeti hili jana, Katibu Mkuu
wa Yanga, Beno Njovu alisema mpaka sasa
hakuna mchezaji aliyefukuzwa isipokuwa kuna
baadhi yao walienda kupumzika wakidai kuwa
wanaumwa.
“Inasikitisha sana kuona baadhi ya watu
wanasema tumewafukuza wachezaji, jambo
ambalo si la kweli, wachezaji wote bado tunao
na tutaendelea kuwatumia katika mechi
zilizobaki,” alisema Njovu.
Alisema ukweli ni kwamba Athumani Idd ‘Chuji’
alitoa taarifa kwa kocha wake kwamba
anaumwa tangu juzi hivyo alishindwa kushiriki
kwenye kambi ya Bagamoyo kwa ajili ya
maandalizi ya mechi ijayo dhidi ya JKT Ruvu
itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa
keshokutwa.
Wachezaji wengine waliotoa taarifa ni Kelvin
Yondani ambaye alidai ana tatizo la kifamilia.
“Yondani alisema ana tatizo akaruhusiwa
kwenda kupumzika, nafikiri pengine ni kwa
sababu alikuwa ana kadi nyekundu hivyo hata
angeshiriki kwenye mazoezi, asingeweza
kucheza mechi ijayo,” alisema Njovu.
Kwa upande wa kiungo Haruna Niyonzima,
alisema bado anaumwa na tatizo lake
linajulikana kwa muda hivyo alipewa ruhusa
kabla
hata ya mechi ya wiki iliyopita.
Alisema wachezaji wengine wote wako
kambini wakiendelea na mazoezi ya kujifua
tayari kwa mechi ijayo ambayo kama nyingine
zilizobaki, ni muhimu kwa mabingwa hao
watetezi.
Tangu kufungwa na Mgambo JKT kwa mabao
hayo 2-1 ambayo Kocha Msaidizi wa Yanga,
Charles Boniface Mkwasa, aliyafafanisha na
zawadi, kumekuwapo na maneno
yanayomhusisha kipa Juma Kaseja na mlinzi
Yondani na tuhuma za kucheza chini ya
kiwango.
Wednesday, April 2, 2014
Yanga kuipeleka TFF kizimbani
WADHAMINI wa Yanga wametoa maelekezo
kwa mawakili wao kuweka pingamizi katika
Mahakama ya Kazi kuzuia mali zao kushikiliwa
na Shirikisho la Soka Tanzania(TFF) bila wao
kuhusishwa katika mchakato.
Hivi karibuni TFF ilisema imepokea amri ya
Mahakama Kuu (Kitengo cha Kazi) kukamata
Sh milioni 106 za Yanga kutokana na mapato
ya mlangoni kwenye mechi zake ili kuwalipa
waliokuwa wachezaji wake Stephen Malashi
na Wisdom Ndlovu, agizo ambalo TFF
imeshaanza kulitekeleza.
Wachezaji hao waliingia mkataba na Yanga
mwaka 2010, lakini Yanga ilivunja mikataba
yao na hivyo kuamua kufungua kesi
mahakamani kupinga suala hilo na kutaka
walipwe haki zao ambapo mahakama
ikaamuru walipwe Sh milioni 106.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa vyombo
vya habari jana na kusainiwa na Katibu Mkuu
wa Yanga, Beno Njovu, sheria ya usajili wa
wadhamini Cap. 318 na kanuni za kesi za
madai zote zinatakiwa kuwa kama mali zozote
zilizo chini ya wadhamini hivyo wanatakiwa
kuuhusishwa katika mchakato wa kesi hiyo.
“Wafaidika hawawezi kwa mujibu wa sheria
kushtakiwa mahakamani wakati wao ni
wafaidika tu wa mali zilizo chini ya udhamini,”
ilisema taarifa hiyo.
Pia, ilisema wadhamini hao wamewapa
maelekezo mawakili kufanya maombi
yanayohitajika kwa Majaji wa Mahakama ya
Kazi kuomba marejeo ya mwenendo wa kesi
na namna gani sheria iliweza kupindishwa
katika Baraza la Usuluhishi na Uamuzi na
kuona hatua gani za kurekebisha hali hiyo
zinaweza kuchukuliwa.
Taarifa hiyo ilisema wachezaji wote wawili ni
watu wasio na makazi ya kudumu na kwamba
mmojawao ameshawahi kulipwa kupitia TFF na
haijawahi kutiliwa maanani na kuongeza:
“Yanga inaamini Jaji wa Mahakama Kuu
akiongozwa vizuri atatoa nafuu stahiki”.
Taarifa hiyo ilisema, wameamua kupeleka
malalamiko yao kwa Jaji Mkuu wa Tanzania ili
kuona kama utaratibu wa kiutawala ulifuatwa
na kutekelezwa kwa usahihi pamoja na
kutokuwepo kwa faili la Mahakama ambalo
lilikuwa tayari katika Mahakama ya Rufaa
kutokana na kuwepo kwa maombi mawili
namba 163 ya mwaka 2013 na 165 ya mwaka
huo.
Ilisema wakati maombi namba 163 yalifutwa
mwaka huo, mengine hayajaitwa kwa ajili ya
kusikilizwa au kufutwa. Taarifa hiyo ilifafanua,
wadhamini ndio wamiliki wa mali zote za
Yanga bila kujali kuwa zisizohamishika,
zinazohamishika au fedha hivyo kuhoji ni kwa
namna gani TFF inaruhusu utekelezaji wa amri
dhidi ya klabu na si wadhamini.
“Sisi tunathubutu kusema kwamba TFF
ilipaswa kuijibu Amri ya Mahakama kwamba
wao hawana fedha ya klabu ambao ni
wafaidika,” alisema. “Hatua ya kuruhusu fedha
za wadhamini kushikiliwa ni kinyume cha
sheria hivyo tunaitaka irudishe fedha hizo
pamoja na riba yake au itufikishe mbele ya
vyombo vya sheria kwa matumizi mabaya ya
fedha za wadhamini."
Tuesday, April 1, 2014
cavani kutua mancherster united au chelsea?
Psg itamwachia huru cavani mwisho wa msimu huu na kuuzwa sasa timu ya moyes na mourinho ndio zipo speed kutaka kumpata.