Friday, June 27, 2014

mla nyama za watu uwanjani huyu hapa

ni luis  suarez..

Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Uruguay Luis
Suarez amefungiwa mechi tisa na shirikisho la
kandanda duniani Fifa baada ya kupatikana na hatia
ya kumng'ta mlinzi wa timu ya Italia Giorgio Chiellini
kwenye mechi yao ya kombe la dunia nchni Brazil.

mla nyama za watu uwanjani huyu hapa

ni luis  suarez..

Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Uruguay Luis
Suarez amefungiwa mechi tisa na shirikisho la
kandanda duniani Fifa baada ya kupatikana na hatia
ya kumng'ta mlinzi wa timu ya Italia Giorgio Chiellini
kwenye mechi yao ya kombe la dunia nchni Brazil.

Thursday, June 12, 2014

MABOMU YARINDIMA MJI WA SAO PAULO .

Polisi katika mjini wa São Paulo nchini Brazil
wametumia mabomu ya machozi kutawanya
waandamanaji wanaopinga Kombe la Dunia, ikiwa
ni saa chache tu kabla ya michuano hiyo kuanza.
Taarifa zinasema mtu mmoja amekamatwa na
mwandishi mmoja wa CNN kujeruhiwa.
Waandamanaji wanasema wamepanga
kuandamana karibu na uwanja ambao shughuli ya
ufunguzi itafanyika.
Maandamano zaidi yamepangwa katika miji
mingine ya Brazil kupinga michuano hiyo
kuandaliwa nchini humo.
Picha za TV kutoka São Paulo zinaonesha polisi
wa kutuliza ghasia wakitumia mabomu ya
machozi na risasi za mpira karibu na uwanja wa
Corinthians.
Waandamanaji hao wamekuwa wakiimba-
wakisema "hakutakuwa na kombe hapa".

Tuesday, June 10, 2014

RATIBA KOMBE LA DUNIA (MDA NI KWA MAJIRA /MASAA YA AFRIKA MASHARIKI)

12-6-2014

23:00 Croatia v Brazil

13-6-2014

19:00 Cameroon v mexico
22:00 Holand v Spain
01:00 Chile v Australia

14-6-2014

19:00 Colombia v Greece
22:00 C.Rica v Aruguay
01:00 England v Italy
04:00 Japan v cote d voire

15-6-2014

19:00 Switzerland v Ecuador
22:00 France v Honduras
01:00 Argentina v Bosnia

16-6-2014

19:00 German v Portugal
22:00 Iran v Nigeria
01:00 Ghana V USA

17-6-2014

19:00 Belgium v Algeria
22:00 Mexico v Brazil
01:00 Rusia v Korea

18-6-2014

19:00 Holand v Australia
22:00 Chile v Spain
01:00 Cameron v Croatia

19-6-2014

19:00 Cote devir v Colombia
22:00 England v Portugal
01:00 Japan v Greece

20-6-2014

19:00 C.Rica v Italy
22:00 Switzerland v France
01:00 Ecuador v Honduras

21-6-2014

19:00 Argentina v Iran
22:00 Ghana v German
01:00 Nigeria v Bosnia

22-6-2014

19:00 Belgium v Russia
22:00 korea v Algeria
01:00 Portugal v USA

23-6-2014

19:00 Chile v Holland
19:00 Australian v Spain
23:00 Cameron v Brazil
23:00 Croatia v Mexico

24-6-2014

19:00 Italy v Greece
19:00 C.rica v England
23:00 Colombia v Japan
23:00 Greece v cote voire

25-6-2014

19:00 Argentina v Nigeria
19:00 Bosnia v Iran
23:00 Switzerland v Honduras
23:00 Ecuador v France.

26-6-2014

19:00 Ghana v Portugal
19:00 USA v German
23:00 Belgium v korea
23:00 Algeria v Russia

Monday, June 2, 2014

HAYA NI MAMBO 21 USIYOYAFAHAMU KUHUSU KOMBE LA DUNIA

1. The tournament has been held 18 times
since 1930, however, only seven different
nations have lifted the trophy.
2. No country from outside South America or
Europe has ever won the World Cup.
3. Five-time champions Brazil are the only
World Cup winners who have not won the title
on home soil.
4. Oliver Kahn of Germany is the only
goalkeeper to have won the Golden Ball (best
player at the tournament) trophy.
5. During the inter-war years, Italian football
Chief Ottorino Barassi secretly took the Jules
Rimet trophy home from a bank in Rome and
kept it under his bed in a shoebox to ensure
Hitler and his Nazi troops didn’t find it. There it
stayed until the 1950 World Cup.
6. The largest crowd for a World Cup match
was in the 1950 final between hosts Brazil and
Uruguay, when 199,954 people filed into the
Maracana in Rio de Janeiro (the host venue of
this year’s final). Uruguay won the match 2-1.
7. Korea Republic became the best performing
Asian nation when it reached the 2002 semi-
finals on home soil.
8. Australia will be the lowest-ranked nation at
this year’s tournament – the Socceroos
currently sit at 59 on FIFA’s world rankings.
9. Tim Cahill is the only Australian player in the
current squad to have scored a World Cup goal.
10. In 2010, New Zealand finished the
tournament as the only undefeated side after
drawing all of its matches. Eventual winners
Spain suffered a shock 1-0 defeat to
Switzerland in the group stage.
11. In 2002, France became the worst ever
defending champions when they were
eliminated in the group stages without scoring
a goal.
12. In 1994, 42-year-old Roger Milla from
Cameroon became both the oldest goal-scorer
and oldest player in World Cup history.
13. Sir Viv Richards is the only person to have
played in both the FIFA World Cup and the ICC
World Cup (cricket).
14. Diego Maradona knocked England out of the
1986 tournament when he punched the ball into
the goal. Maradona famously said it was “the
hand of God”.
15. Brazil hosted one of the most unique
editions of the World Cup in 1950 as it was the
only tournament in which the winner was
determined by a final group stage, with the final
four teams playing in a round-robin format,
instead of a knockout stage.
16. During a time dominated by the iconic
Brazilian Pele, Just Fontaine won the Golden
boot at the 1958 World Cup in Sweden by
scoring a total of 13 goals in the tournament.
The French striker scored 13 in just six
matches - the highest number of goals ever
scored by one player at a single World Cup
tournament.
17. Italy's triumph in 1934 is said to be
influenced by military leaders seeking
propaganda coups. At the time, fascist dictator
Mussolini was in power in Italy. Mussolini
decided  to have dinner with just the referee
and linesman instead of the usual dinner
involving players and staff members from both
teams on the night before the final. Italy came
out victorious as they defeated Czechoslovakia
2-1.
18. Italy has always been a major contender to
lift the trophy in every tournament they have
featured in, but while they won back to back
World Cups in 1934 and 1938, the Italians had
to wait 44 years for their third title.
19. Which player has scored the most goals in
a single World Cup match? No, it isn't Pele,
Maradona, Gerd Muller or Ronaldo. Oleg
Salenko, who represented Russia at the 1994
World Cup finals in USA, scored 5 goals against
Cameroon which stands as the record for the
most goals by an individual in a World Cup
game.
20.  Hungary beat El Salvador 10-1 on June
15,1982 in Elche, Spain, thus recording the
biggest scoreline in the tournament finals.
21.  A crowd search by police before 1930’s
World Cup final in Uruguay led to the
confiscation of 1,600 revolvers.

UCHAGUZI YANGA:Sasa ni hadi 14 June mwakani

UCHAGUZI Mkuu wa Yanga umesogezwa
mbele hadi Juni 14 mwakani huku wanachama
wakimtaka Mwenyekiti wao Yusufu Manji
kuwania tena nafasi hiyo kwa kipindi cha
miaka minne au minane endapo itakubaliwa
kwenye Katiba.
Awali, Uchaguzi Mkuu wa Klabu hiyo
ulipangwa kufanyika Juni 15 mwaka huu, lakini
wanachama wa Yanga waliokuwa na mkutano
wa marekebisho ya Katiba jana kwenye
ukumbi wa Polisi Osterbay waliamua uchaguzi
huo usogezwe mbele ili kupisha marekebisho
ya Katiba.
Aidha, wanachama wa klabu hiyo wamepitisha
vipengele viwili vilivyoongezwa kwenye Katiba
yao kimoja kikiwa ni kuunda Kamati ya Maadili
kilichopendekezwa na Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF) lakini wakihitaji marekebisho
badala ya Kaimu Mwenyekiti iwe Makamu
Mwenyekiti.
Aidha, wanachama wameipa mamlaka Kamati
ya Utendaji kufanya nyongeza ya mabadiliko
katika Katiba ya Yanga endapo itahitajika na
TFF ndani ya miezi isiyozidi mitatu kuanzia
tarehe ya jana bila kuitisha mkutano wa
wanachama.
Katika mkutano huo, Manji alitangaza kwa
wanachama kuwa hatogombea nafasi hiyo kwa
mara nyingine, jambo ambalo wanachama
hawakukubaliana naye.
Baada ya kauli hiyo, Mwenyekiti wa Baraza la
Wazee la Yanga Jabir Katundu alihoji
wanachama kama wanakubaliana naye, jibu la
hapana likatawala, wakimuomba aendelee na
ndipo akaamua kupisha mjadala dhidi yake
ufanyike kwa haki huku yeye akitoka nje.
Katika mjadala huo ulioongozwa na Mwenyekiti
wa Baraza la Wadhamini wa Yanga Fatuma
Karume na mjumbe Francis Kifukwe
wanachama walikubali kwa pamoja agombee
na ndipo Manji alipoitwa kuelezwa msimamo
wa wanachama.
Wanachama wengi walipendekeza akae
madarakani kati ya miaka minne au minane
baada ya kufanikiwa kurejesha imani ya
wanachama na kuwezesha pia, Yanga
kumaliza Ligi ikiwa na tuzo ya nidhamu.
Kwa mujibu wa Katiba ya Yanga uongozi
unakaa kwa miaka minne kabla ya kufanyika
uchaguzi mkuu, lakini wanachama
wamependekeza muda wa ukomo wa uongozi
uingizwe kwenye Katiba kwamba ni miaka
minane jambo ambalo Manji alisema linatakiwa
kuingizwa kwenye Katiba.
Pia, wanachama hao walipendekeza badala ya
kuitwa Mwenyekiti, awe Rais jambo ambalo
linahitaji kufanyiwa marekebisho ya Katiba
ndipo likubalike.
Baada ya Manji kuitwa kwa ajili ya kukubali
ombi la wanachama hao alisema:
“Siwezi kusema hapana kwa mama wa Taifa
(Fatma ambaye ni mke wa Rais wa Kwanza wa
Zanzibar Abeid Karume), naona aibu
kumkatalia kwa sababu ataona kuwa
nimemdharau, nashukuru kwa imani yenu
kwangu, naomba mnipe muda, uchaguzi
usogezwe mbele kwa mwaka mmoja sababu
ya marekebisho ya Katiba kisha mengine
yafuate,” alisema.
Alisema nia ya kusogeza mbele ni kutoa nafasi
ya katiba hiyo kuingiza baadhi ya
mapendekezo yaliyotolewa na wanachama hao
na kwamba hadi Katiba ikubalike kwa msajili,
uchaguzi utangazwe siku 60 muda utakuwa
umeenda kwani wakati huo atakuwa akihitajika
kocha mpya na timu itakuwa kwenye
maandailizi ya Ligi Kuu.
“Nia ya Yanga ni kufanya vizuri katika
michuano ya kimataifa na Ligi Kuu tunahitaji
maandalizi sasa tukisema tufanye uchaguzi
Septemba mwaka huu tutaipeleka Yanga
pabaya,”alisema na kuongeza kuwa sasa
viongozi watakuwa ni wale wale isipokuwa
Kamati ya Utendaji itabadilishwa.
Katika hatua nyingine, Manji alisema kati ya CV
(wasifu) saba za makocha walizopitia kwa ajili
ya kuifundisha Yanga, wamechagua moja ya
Kocha wa zamani wa Taifa Stars Marcio
Maximo hivyo wanaendelea kufanya naye
mazungumzo.
Pia, alisema katika kukiimarisha kikosi hicho
wataongeza wachezaji wawili wa kigeni na
watatu wa nyumbani lengo ni kufanya vizuri
msimu ujao.

UCHAGUZI SIMBA:Saba waenguliwa

KAMATI ya Uchaguzi ya klabu ya Simba, chini
ya Mwenyekiti Dk Damas Ndumbaro,
imewaondoa wagombea saba katika
kinyang’anyiro cha kuwania nafasi ya Ujumbe
wa Kamati ya Utendaji wa klabu hiyo, huku
wagombea wengine watano wakitangaza
kujitoa katika mchakato huo kwa sababu za
kifamilia.
Aidha, mbali na kuwaengua wagombea hao,
Ndumbaro alimzungumzia aliyekuwa mgombea
wa nafasi ya Rais wa klabu hiyo Michael
Wambura na kutaka wanachama
wasiyumbishwe na kauli zake.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar
es Salaam jana, Ndumbaro alisema, katika
mchakato mzima wa usaili, kamati yake
iliongozwa na Ibara ya 26, ambako wagombea
wote saba walioenguliwa walibanwa na vifungu
vidogo vya 2 na 6, hivyo kukosa sifa za kubaki
katika uchaguzi huo.
Kwa mujibu wa Ndumbaro, kifungu kidogo cha
2 kinataka mgombea awe na elimu ya kidato
cha nne anayetambuliwa na Baraza la Mitihani
la Taifa, wakati kifungu cha 6 kinataka
mgombea awe na uanachama wa klabu hiyo
usiopungua miaka mitatu na si chini ya hapo.
Ndumbaro aliwataja wagombea waliondolewa
kwa kutokidhi Ibara ya 26 kifungu kidogo cha 2
kuwa ni George Wakuganda na Salim Jazza,
wakati wagombea Ahmed Mlanzi, Emmanuel
Kazimoto, Omary Omary, Ramson Rutiginga na
Selemani Dewji wakishindwa kukidhi Ibara ya
26 kifungu kidogo cha 6.
Aliwataja wagombea waliojitoa katika
kinyang’anyiro hicho kuwa ni Emmanuel
Mayage na Joseph Itang’are ‘Kinesi’
waliokuwa wakiwania nafasi ya Makamu wa
Rais, pamoja na Asha Kigundula, Hussein
Simba na Juma Pinto, waliokuwa wakiwania
nafasi ya Ujumbe wa Kamati ya Utendaji.
“Wagombea waliojitoa, kwetu wameeleza
kufanya hivyo kutokana na sababu za
kifamilia, ambazo kama kamati hatuko huru
kuhoji, zaidi ya kuridhia.Ama kuhusu
waliopitishwa, wapo wanaoweza kuondolewa
kutokana na baadhi ya masuala kufikishwa
mikononi mwa vyombo vya dola,” aliongeza
Ndumbaro.
Alifafanua zaidi Ndumbaro alisema, baadhi ya
wagombea taarifa zao ziko mikononi mwa
vyombo vya dola ambavyo ni Taasisi ya
Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania
(Takukuru) na Baraza la Mitihani la Taifa
(Necta), na kwamba watakaokutwa na makosa
wanaweza kuondolewa kwenye mchakato huo.
Akizungumzia tuhuma za rushwa ya ngono na
pesa zilizoelekezwa kwa kamati hiyo na
mgombea Urais waliyemuondoa, Michael
Wambura, Ndumbaro alisema kuwa
amesikitishwa na tuhuma hizo na maneno
mengine machafu yaliyotolewa na Wambura,
aliyemtaja kama bingwa wa soka la
mahakamani.
Kamati hiyo ya Ndumbaro ilimuengua Wambura
kuwania nafasi ya rais kwenye uchaguzi huo
kwa madai ya kuwa si mwanachama halali wa
Simba.
“Wanachama Simba wasiyumbishwe na kauli
za Wambura, Kamati haijamuonea wala
haijapokea rushwa ya ngono na pesa
kupindisha sheria. Huyu ni wa kupuuzwa,
kwani kama angekuwa muelewa, alipaswa
kukata rufaa na sio kupakana matope kwa
tuhuma zisizo na ushahidi,” alisema
Ndumbaro.
Ndumbaro alisisitiza kuwa, katika kanuni za
Fifa, TFF na hata Simba zinakataza soka
kupelekwa katika mahakama za kawaida,
hivyo kitendo alichokuwa amefanya Wambura
hadi kusimamishwa uanachama, kilikuwa
sawa na kifo na wao kama kamati,
walichofanya ni kumzika marehemu ambaye
akiachwa ataoza na kunuka.
Mwenyekiti huyo ambaye pia ni mwanachama
wa Simba alisema Wambura ni tatizo kwenye
soka la Tanzania kutokana na tabia zake za
kupenda kukimbilia Mahakamani mara kwa
mara kitu ambacho ndicho kilichomuua na
ndiyo maana Kamati yake kupitia kanuni
imeamua kummalizia kwa kumzika.
“Mtu huyu mmoja ameshaenguliwa kwenye
chaguzi tatu ikiwemo ule wa TFF na wa Simba
mara mbili huoni kama huyu ni tatizo na
ukitaka kujua kama ni tatizo ndiyo sababu
Jamal Malinzi (Rais wa TFF) hajamteua katika
kamati hata moja kati ya 18
alizoziunda,”alisema Ndumbaro.
Ndumbaro pia alisema hawezi kushindana na
Wambura kwa sababu ni mwanafunzi wake
aliyewahi kumfundisha somo la Sheria Chuo
Kikuu Huria cha Dar es Salaam.
Kwa upande wake, Mjumbe wa Kamati hiyo
Amin Bakhressa, alikiri kushtushwa na madai
yaliyotolewa na Wambura kuwa Kamati yao
imeshiriki kupokea rushwa ya ngono na pesa,
hivyo kumtaka mlalamikaji huyo kuthibitisha
tuhuma kwa kumtaja aliyetoa na kupokea
rushwa hizo miongoni mwao, ili wajiwajibishe.
“Tunamuomba athibitishe, vinginevyo
akanushe kwa uzito ule ule aliotoa, kwani
kimsingi tuhuma hizi zimechafua hali ya hewa
hadi ya kifamilia kwa kutuhusisha na tuhuma
za ngono, ambazo kwa weledi na heshima
walizonazo wajumbe wa kamati hii, hawawezi
kushiriki upuuzi huo hata mara moja,”
alisisitiza Bakhressa.

Taifa stars iyoooooooo....

TIMU ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars jana
ilifanikiwa kufuzu raundi ya pili ya kuwania
kufuzu fainali za kombe la Mataifa Afrika
baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 na
Zimbabwe katika mchezo mkali wa marudiano
uliofanyika jijini Harare.
Kwa matokeo hayo Stars imefuzu kwa ushindi
wa jumla ya mabao 3-2 baada ya kushinda
bao 1-0 katika mechi ya awali iliyofanyika Dar
es Salaam wiki mbili zilizopita kwa bao
lililofungwa na John Bocco dakika ya 36. Stars
sasa itacheza na msumbiji iliyoitoa Sudani
Kusini kwa jumla ya mabao 5-0.
Kwa mujibu wa blog ya
bongostaz.blogspot.com Zimbabwe ndiyo
waliokuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza
katika dakika ya tatu ya mchezo lililofungwa na
Danny Phiri kufuatia shambulizi kubwa kwenye
lango la Stars na kujipatia bao hilo ambalo
lilifufua matumaini ya Wazimbabwe kusonga
mbele.
Hali iliwabadilikia ghafla Wazimbabwe baada ya
Nahodha wa Stars Nadir Haroub
kuisawazishia Tanzania bao hilo kwa kichwa
akiunganisha kona ya Simon Msuva dakika ya
21 na kufanya matokeo kuwa sare ya 1-1 hadi
mapumziko.
Kipindi cha pili Stars iliyo chini ya kocha
Mholanzi Mart Nooij, ilikianza kwa kasi na
kufanikiwa kupata bao la pili katika dakika ya
46 lililofungwa na Thomas Ulimwengu baada
ya mabeki wa Zimbabwe kudhani ameotea.
Hata hivyo bao hilo la Stars halikudumu kwani
dakika ya 54 wenyeji Zimbabwe,
walisawazisha kupitia kwa Denver Mukamba,
aliyepiga kona iliyoingia moja kwa moja
wavuni.
Bao hilo liliibua ari ya wachezaji wa na kuanza
kucheza kwa kasi na kulisakama lango la
Stars kwa muda mrefu lakini ngome imara
iliyokuwa chini ya Nahodha Haroub kipa
Deogratius Munish na Said Morad aliyeingia
kipindi cha pili ilikuwa makini kwa kuondosha
hatari zote zilizoelekezwa langoni mwao.
Baada ya kuona timu yake inaelemewa zaidi
dakika za mwishoni kocha Nooij aliwatoa
Msuva na Ulimwengu nafasi zao
zikachukuliwa na Moradi pamoja na Mrisho
Ngassa ambao waliongeza uimara na
kufanikiwa kulinda matokeo yasibadilike.