Saturday, May 17, 2014

Atletico Madrid ,mfalme La liga

TIMU ya Atletico Madrid imetwaa kombe la La
Liga baada ya sare ya 1 - 1 dhidi ya Barcelona
kwenye Uwanja wa Nou Camp. Kwa ushindi
huo wamefikisha pointi 90 wakati Barcelona
wakiwa na pointi 87 sawa na Real Madrid
ambao wamemaliza wakiwa nafasi ya tatu.
Mara ya mwisho kutwaa kombe hilo ilikuwa
1996!

Arsenal, bingwa FA cup

Arsenal wametwaa kombe la FA baada ya
kukaa miaka tisa bila kombe lolote . Wametwaa
ndoo hiyo kwa kuifunga Hull City bao 3 -2 katika
muda wa nyongeza baada ya sare ya 2- 2
katika muda wa kawaida kwenye Uwanja wa
Wembley usiku huu .
Wafungaji Arsenal: Carzola dakika ya 17 ,
Koscielny dakika ya 71 na Ramsey dakika ya
109 wakati ya Hull City yakifungwa na Chester
dakika ya 4 na Davies dakika ya 8 .

Wednesday, May 14, 2014

Angalia hapa mpira utakaotumika kwenye mechi za kombe la dunia

Je kifaa hiki kitaweza? Hilo ndilo swali linaloulizwa
na wengi kuhusu Brazuca, jina la mpira rasmi
utakaotumiwa katika dimba la Kombe la Dunia
lijulikanalo kama Brazil 2014.
Mpira huo ni wa 12 kuundwa na kampuni ya Adidas
kwa kinyang'anyiro cha Kombe la Dunia.
Kampuni hiyo ilikosolewa miaka minne iliyopita juu
ya mpira uliojulikana kama Jabulani, mpira rasmi
wa Kombe la Dunia wa mwaka 2010 Afrika Kusini.
"hauna mwelekeo angani na hautabiriki," ndivyo
alivyosema mlinda lango wa Italia Gianluigi Buffon,
naye mshambulizi wa Brazil Luis Fabiano alisema
mpiro huo ulikuwa wa "kimiujiza".
Adidas sasa inadai kuwa Brazuca imeimarisha
mguzo wake na shabaha.
" Tumefanya uchunguzi unaohusiana na mwendo
wa mpira huu na matokeo yanaonyesha kuwa
unasafiri na kupaa kwa njia zinazotarajiwa na
kujipinda kokote ni kudogo sana hivi kwamba
hakutambuliki," mkurugenzi wa kandanda wa
Adidas Matthias Mecking aliambia BBC.
Wataalamu wa kasi angani waliohojiwa na BBC
walisema kuwa kuna sababu tatu zitakazotumiwa
kuamua matumizi ya mpira wa Kombea la Dunia la
Brazil 2014.
"jambo muhimu sana kwa mpira huo ni jinsi ulivyo
"Kitu muhimu sana kuhusu mpira ni mguso wake,''
alieleza Daktari Rabi Mehta, afisa mkuu katika kituo
cha utafiti wa mambo ya anga za juu nchini
Marekani.
Daktari Rabi Mehta, aliambia BBC kuwa amefanya
majaribio ya mpira ya Jabulani katika shimbo lenye
hewa na amekuwa akichunguza Brazuca nao.
Anasema kuwa hali ya kukosa mwelekeo hutokea
wakati mpira hauzunguki au ukizunguka polepole
sana.
Mehta anasema mpira ulipokua laini unapopaa
kwenye anga bila kuzunguka, hewa iliyo karibu nao
inaingilia maeneo ambako ngozi inakutana na
kusabisha mpira kupata mwelekeo tofauti.
Ingawa mshambulizi matata wa Brazil Luis Fabiano
(kushoto) ameutaja huo mpira wa 2010 kama wa
kimiujiza lakini Daktari Mehta anasema kwa
kufanya mpira huo usiwe laini ni kama "tumerejea
tulikokuwa."
Baadhi ya wachezaji waliwahi kulalamika kuhusu
mpira wa Jabulani uliotumiwa Afrika Kusini
Mipira isiyo laini husafiri mwendo mrefu zaidi. Mpira
unapopaa hewani, huchochea na kusukuma hewa,
jinsi mashimo madogo yaliyoko kwenye mpira wa
gofu, Daktari Simon Choppin anasema.
"Hali hiyo ya kuchochea ni muhimu kwa kasi na
mwendo wa kutegemewa. Mpira ulio laini kabisa
hukabiliana na upepo mwingi na kuvuruga mwendo
wa hewa, " Bwana Choppin anasema.
Je uamuzi wa wanasayansi ni upi?
"nina hakika kuwa Brazuca utakuwa na tabia sawa
na ule wa asili ulio na vipande 32 vilivyoshonwa
kama hapo awali kwa hivyo malalamiko kama yale
tuliyotolewa katika mashindano mawili yaliyopita ya
Kombe la Dunia yatapunguka," Rabi Mehta alisema.

Sunday, May 11, 2014

man city bingwa epl

Congratulations Manchester City, 2013/14 Barclays Premier League champions

Saturday, May 10, 2014

Wambura nae yumo,mbio za urais Simba

KUMEKUCHA Simba. Ndivyo unavyoweza
kueleza baada ya jana mmoja wa wanachama
wake maarufu kutangaza kuwania urais katika
Uchaguzi Mkuu wa Juni 29, mwaka huu.
Michael Richard Wambura amesema Jumatatu
ijayo atakwenda katika makao makuu ya
Simba, Mtaa wa Kariakoo, Dar es Salaam
kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo ya juu
katika uongozi wa klabu hiyo.
“Nimeulizwa sana (na waandishi wa habari)
kama nitawania uongozi katika Uchaguzi Mkuu
ujao. Jibu langu ni ndiyo. Jumatatu ijayo saa
tano asubuhi, nitakwenda kuchukua fomu ya
kuwania Urais wa Simba,” alisema Wambura
alipozungumza na gazeti hili jana.
Kiongozi huyo wa zamani wa soka katika
Simba na Shirikisho la Soka (TFF) wakati huo
Chama cha Soka Tanzania (FAT), alisema
ataeleza sababu za kuwania nafasi hiyo baada
ya kuchukua fomu siku hiyo.
“Nitaeleza sababu za kuwania nafasi hiyo
baada ya kuchukua fomu,” alieleza Wambura.
Uchaguzi Mkuu wa Simba umepangwa
kufanyika Juni 29, mwaka huu na fomu kwa
nafasi mbalimbali za uongozi zilianza kutolewa
jana hadi Mei 14, mwaka huu saa 10 jioni.
Mbali ya Wambura, jina jingine linalotajwa
katika kuwania urais wa Simba ni
mwanachama maarufu katika Kundi la Friends
of Simba, Evans Aveva ambaye anatajwa
kuungwa mkono na kundi hilo.
Wambura, ambaye amewahi kuwa Mjumbe wa
Baraza la Michezo la Taifa (BMT), pia
amewahi kuwa Katibu Mkuu wa FAT na
baadaye TFF, kabla ya kushindwa na Leodegar
Tenga katika Uchaguzi Mkuu wa TFF, mwaka
2005.
Baadaye alikuwa Katibu Mkuu wa Simba. Rais
wa sasa wa Simba, Alhaj Ismail Aden Rage
ametangaza kutowania kiti hicho.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya
Uchaguzi, Dk Damas Ndumbaro, nafasi
zitakazowaniwa ni Rais, Makamu wa Rais na
wajumbe watano wa Kamati ya Utendaji,
mmoja lazima awe mwanamke.
Kamati hiyo itakutana Mei 17, mwaka huu
kufanya uhakiki wa fomu za wagombea, na
Mei 19 watatangaza majina ya wagombea
walioomba nafasi hizo. Fomu zitatolewa kwa
nafasi ya Rais Sh 500,000, Makamu wa Rais
Sh 300,000 na wajumbe Sh 200,000.
Aidha, Mei 20 hadi 22, itakuwa ni siku ya
pingamizi dhidi ya wagombea na wanaotakiwa
kuweka pingamizi ni lazima wawe wanachama
wa klabu hiyo.
Mei 25 wataanza kusikiliza pingamizi, Mei 27
kutoa uamuzi, Mei 29, usaili wa wagombea na
Mei 30, itakuwa ni siku ya kutangaza matokeo
ya usaili.
Kuanzia Juni 2 hadi 9, Kamati ya Maadili na
wadau wataangalia masuala ya kimaadili na
Kamati ya Rufaa itakuwa inasikiliza rufaa
wakati maamuzi yote yatakuwa Juni 10 hadi 12
na kusikiliza rufaa hizo ni Juni 8-12.
Juni 13 hadi 15, itakuwa ni kukata rufaa Kamati
ya Rufaa ya Maadili, na Juni 16-20 kusikiliza
rufaa hizo, wakati Juni 21-23 maamuzi ya
mwisho ya kamati hiyo na siku inayofuata
orodha ya mwisho ya wagombea itatangazwa,
kabla ya kuanza kampeni kuanzia Juni 24 hadi
28.

Ngorongoro kukipiga na Nigeria leo

TIMU ya soka ya vijana chini ya umri wa
miaka 20 ‘Ngorongoro Heroes’ leo itakuwa
kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam
kumenyana na wenzano wa Nigeria katika
mechi ya raundi ya pili ya kuwania kucheza
michuano ya Mataifa Afrika kwa vijana wa umri
huo.
Ngorongoro imefuzu raundi hiyo baada ya
kuiondosha Kenya kwa mikwaju ya penalti.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF) mechi hiyo itaanza saa
kumi jioni.
Akizungumzia mechi hiyo, kocha wa
Ngorongoro Heroes John Simkoko alisema
anaamini atapata matokeo mazuri leo licha ya
kukiri kuwa mechi hiyo ni ngumu.
“Nigeria tunawajua ni wazuri lakini hata sisi
pia tuna timu nzuri na tumejiandaa kukabiliana
nao,” alisema Simkoko.
“Nimekaa kambini na wachezaji wangu na
kwenye mazoezi nawaona wanavyofuata
maelekezo yangu, naamini hatutawaangusha
kesho (leo),” alisema.
Fainali za 19 za Mataifa Afrika, zimepangwa
kufanyika Senegal mwakani ambapo
zitashirikisha timu saba zitakazofuzu kwenye
mechi za mchujo kabla ya kuungana na
wenyeji Senegal watakaofanya jumla ya timu
nane kwenye michuano hiyo.
Tanzania haijawahi kufuzu michuano hiyo
tangu ilipofanya hivyo mwaka 1980 ambapo
timu ya wakubwa ilifuzu katika michuano
iliyofanyika Lagos, hata hivyo iliishia kwenye
makundi.
Viingilio katika mechi hiyo ni Sh 2,000 kwa
sehemu zote wakati upande wa VIP itakuwa
Sh 5,000. Kwa mujibu wa TFF, tiketi zitaanza
kuuzwa leo asubuhi kwenye magari maalumu.

Wednesday, May 7, 2014

kikosi cha brazil 2014

Brazil's World Cup squad:
Goalkeepers: Julio Cesar (Toronto FC/CAN),
Jefferson (Botafogo), Victor (Atletico Mineiro)
Defenders: Dante (Bayern Munich/GER), David
Luiz (Chelsea/ENG), Henrique (Napoli/ITA),
Thiago Silva (PSG), Daniel Alves (Barcelona/ESP),
Maicon (Roma/ITA), Marcelo (Real Madrid/ESP),
Maxwell (Paris St Germain/FRA)
Midfielders: Fernandinho (Manchester City/ENG),
Hernanes (Inter Milan/ITA), Luiz Gustavo
(Wolfsburg/GER), Oscar (Chelsea/ENG), Paulinho
(Tottenham/ENG), Ramires (Chelsea/ENG), Willian
(Chelsea/ENG)
Strikers: Bernard (Shakhtar Donetsk/UKR), Fred
(Fluminense), Hulk (Zenit Saint-Petersburg/RUS),
Jo (Atletico Mineiro), Neymar (Barcelona/ESP)